1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

DW yatimiza miaka 65 tangu kuundwa

4 Juni 2018

Katika wakati ambapo dunia inakabiliwa na migogoro mbalimbali na kuongezeka kwa siasa kali za mrengo wa kulia, shirika la utangazaji wa kimataifa la Ujerumani Deutsche Welle linajikuta likikabiliwa na changamoto mpya.

https://p.dw.com/p/2yvJM
Headerbanner 65 Jahre DW Deutsch

"Wapenzi wasikilizaji  katika  nchi  za  mbali ...." Ni  maneno  kutoka  kwa kiongozi wa  nchi. Kwa  salamu  hizo  kutoka  kwa  rais  wa  Ujerumani Theodor Heuss  DW  ilianza  rasmi  tarehe  3,Mei  mwaka  1953 kurusha  matangazo  yake. Ilikuwa  dhahiri  kwamba mwanzoni  mwa matangazo  hayo , "msikilizaji   katika  nchi za  nje  aliweza  kupata taswira ya  kisiasa , kiuchumi  na  kiutamaduni    ya  Ujerumani."  Kwa matangazo ya  mawimbi  ya  masafa  mafupi DW  kutoka  Kolon ilifanikiwa  katika  lengo  lake  na  kuwafikia  pekee  katika  lugha  ya Kijerumani wasikilizaji  katika  maeneo  mengi ya  dunia.

Global Media Forum 2016 Peter Limbourg
Mkurugenzi wa DW Peter LimbourgPicha: DW/M. Müller

Mwaka  1954 ndipo  yalianza   matangazo  ya  baadhi  ya  lugha  za kigeni. Mwaka  1992  matangazo  ya  televisheni  yakaanza, na  mara baada  ya  hapo DW  ikaanza  kusambaza  habari  pia  kwa  njia  ya mtandao. Deutsche  Welle  imebadilika,"  baada  ya  miaka  65 amesema  mkurugenzi  Peter  Limbourg. "Kutoka  kuwa  kituo  cha utangazaji kinachorusha  matangazo  yake  kwa masafa  mafupi  nje  ya nchi  na  kuwa  shirika  la  kimataifa  la  habari,  ambapo  lugha  30 zinarusha  hewani  matangazo  yake,  ambapo tunajaribu  kwa  kila linalowezekana  kuwafikia  watu kwa  kila  hali, kuwapatia  taarifa ambazo  katika  nchi  zao  huchujwa  kwanza   ama  kuzuiwa  kabisa. Ni mabadiliko  makubwa   katika  miaka  hii  65." Bila  shaka   ilikuwa  rahisi katika  enzi  zile  za  kurusha  matangazo  kwa  masafa  mafupi kuwafikia  wasilikizaji  katika  kila  kona  ya  dunia. "Lakini  iwapo tusingebadilika, sijui  tungekuwa  wapi."

Deutschland Bundespresseball 1955 - Bundespräsident Theodor Heuss
Rais wa Ujerumani Theodor Heuss (kushoto) na waziri wa fedha wa wakati huo Fritz Schäffer (kulia)Picha: picture-alliance/dpa

Leo  hii kwa  mujibu  wa  mkurugenzi  wa  DW utendaji  wa  hayo  yote ni  mgumu.  Kwa  hivi  sasa  kuna  fursa  nyingi  za  kuwafikia wasikilizaji  wengi  zaidi  kuliko  hapo  awali  kwa kupitia  mtandao  wa internet, mitandao  ya  kijamii  na  mfumo  wa  kuwa  na  redio washirika. Mkurugenzi  anasema matangazo  ambayo  ni  mchanganyiko wa  taarifa  ya  habari, uchambuzi  na  msingi  wa  habari  yenyewe, utangazaji  wa  kisasa  ambao  unawagusa  wasikilizaji  wa  rika  mbali mbali, na  mara  nyingi  zikilenga  katika  kundi  la  vijana  zaidi. Limbourg amekuwa  kiongozi  wa  shirika  hilo  la  DW   kwa  muda  wa  miaka karibu  minne  na  nusu  sasa  na  anataka kuimarisha  umuhimu  wa matangazo  ya  kimataifa.

DW MA-Bild Anna Higgins
Baadhi ya wafanyakazi wa DWPicha: DW/P. Böll

Sherehe  bungeni

Jumanne  hii kutakuwa   na  sherehe  maalum  katika  bunge  la Ujerumani  Bundestag za  miaka  65  tangu  kuanzishwa  kwa matangazo  ya  shirika  hilo  la  utangazaji. Watakaohudhuria  ni  pamoja na  waziri  wa  utamaduni  Monika Gruettes  pamoja  na  wabunge kadhaa  wa  makundi  yote  ya  vyama. Hususan  mgeni  rasmi  atakuwa kansela  wa  Ujerumani Angela  Merkel, ambaye  atalihutubia  bunge. Na kansela  anajifahamisha  kuhusiana  na  mradi  wa  hivi  sasa  wa matangazo,  ambao  ni  kuhusu uelekezi  wa  vidio  katika  lugha  ya Kirusi , ambao  utasaidia , kuzuwia  habari  za  uongo.

Tafsiri  hali  ya  "matangazo  haya"  ni  pana: Matangazo  ya  televisheni katika  lugha  nne, taarifa  katika  mtandao  wa  internet  kwa  lugha  30 pamoja  na  shughuli  mbali mbali  katika  mitandao  ya  kijamii. Simu za mkononi  za  kisasa  zina  umuhimu  mkubwa  katika   kupashana habari.  Msikilizaji wa  kweli  katika  enzi  hizi  kwa  kiasi  kikubwa  ni kijana.

Kile  ambacho Wajerumani  hawakijui ni  kwamba  Kituo  cha  mafunzo cha  DW , zamani  shirika la  kimataifa  la  maendeleo  ya  vyombo  vya habari . limefanikiwa  kuwafunza  maelfu  ya  waandishi  habari  tangu mwaka  1965. Kwa  hiyo  mawaziri  wa  Ujerumani  hukutana  na  watu wenye  uwezo  mkubwa  nje  ya  nchi  kwa  ajili  ya  mazungumzo, ambao  wamepata  mafunzo  katika  chuo  hiki cha  DW.

CDU Kanzlerin Angela Merkel
Kansela wa Ujerumani Angela MerkelPicha: picture-alliance/dpa/C. Schmidt

Baadhi ya  masuala  mengine  magumu  ya  kisiasa  duniani yanafanana na  wakati  wa  kuundwa  kwa  DW  miaka  65  iliyopita. Baadhi  ni  pamoja  na  matamshi  ya  wakati  wa  enzi  za  vita  baridi, kutoa mawazo  pamoja  na  uhuru  wa  vyombo  vya  habari  umo hatarini. Wakati  umekuwa  mgumu  sana , ikiwa  na  maana  kazi  nyingi zaidi  kwa  DW.

Changamoto za enzi  hizi

Tunapaswa  kutoa  taarifa, kujenga  madaraja  na kusambaza maadili, " amesema  mkurugenzi  mkuu  wa  DW  Limbourg. Iwapo tutaiita  enzi  ya  sasa  ya  vita  baridi  ama  utaratibu  wa mtengano  duniani, changamoto  kupitia  propaganda , tarifa za  uongo, uhamiaji, mabadiliko  ya  tabia  nchi  na  ugaidi  vinaongezeka.

Moderne Berufe, die wir der Digitalisierung verdanken
Mtandao wa Internet unatumika zaidi na vijanaPicha: picture-alliance/dpa Themendienst/J. Kalaene

Limbourg  anazungumzia  pia kuzuiwa  kwa kiasi  fulani  kwa  matangazo ya  DW  nchini  China  ama  Iran. "Hali  hii  inatutia  wasi  wasi , lakini hali  hii  inaonesha  pia, kwamba  kazi  yetu ina athari chanya."  Leo hii kuna  mapambano  ya kimifumo  na  kinadharia  pamoja  na  mbio  za mashindano  ya  matangazo  kimataifa. 

"wafanyakazi  ndio  ufunguo  wa  mafanikio  ya  Deutsche Welle", imeelezwa  katika  misingi  ya  DW. Katika  miji  yote ambayo  DW  iko Bonn   na  Berlin  kuna  wafanyakazi  wapatao 3400 kutoka  mataifa zaidi  ya  60 wanaofanyakazi. Kwa  hiyo  DW inamchanganyiko  ya tamduni  nyingi kuliko taasisi  yoyote  nchini  Ujerumani. Idadi  ya waandishi  walioko nje  ya  Ujerumani  katika  bara  la  Afrika, Asia  na Amerika  kusini  inaongezeka. "Mchanganyiko  huu  wa  tamaduni  ni hazina  kubwa  katika  uwezo  wa  matangazo  yetu, anasema mkurugenzi  mkuu  Limbourg.

Mwandishi: Christoph Strack / ZR / Sekione  Kitojo

Mhariri: Iddi Ssessanga