1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

England yaibwaga Scotland kombe la dunia wanawake

Sekione Kitojo
10 Juni 2019

Mashindano ya  fainali  za  kombe  la  dunia  kwa  wanawake, hamasa  yazidi  kuongezeka, England yawaangusha  Scotland

https://p.dw.com/p/3K8qh
FIFA Frauenfußball WM 2019 England - Schottland
Wachezaji wa timu ya taifa ya England Picha: Reuters/E. Gaillard

Mabingwa  wa  zamani  Japan watakuwa  na  matumaini  ya kukimbizana  na mahasimu  wao  katika  kundi  hilo England ambao walianza  kwa  kushinda jana  Jumapili  wakati  kikosi  hicho  maarufu kama  Nadeshiko kikifungua  kampeni  yake  katika  kombe  la  dunia dhidi ya  Argentina leo Jumatatu.

FIFA Frauenfußball WM 2019 England - Schottland
Patashika katika lango la England katika mchezo dhidi ya ScotlandPicha: Reuters/J. P. Pelissier

England  waliwashinda  mahasimu wao  wakubwa  Scotland mjini  Nice jana  Jumapili, licha  ya kikosi hicho  cha  kocha  Phil Neville  kulazimika  kulinda  kwa  njia  zote ushindi  wao  wa  mabao 2-1 kwa  muda  mrefu wa  mchezo huo.Engalnd  ambayo ni  moja  kati  ya  timu  zinazopigiwa  upatu kutoroka  na  taji  hilo, ilinyakua  pointi  zote  tatu  katika  kundi  D katika  mchezo  uliopigwa  kusini  mwa  Ufaransa, lakini Scotland ilibambana  katika  kipindi  cha  pili katika  mchezo  wao  wa  kwanza kushiriki  katika  kombe  la  dunia  na Claire Emslie alipata  bao moja.

FIFA Frauenfußball WM 2019 Brasilien -Jamaika
Wachezaji wa timu ya taifa ya wanawake wa Brazil wakishangiria bao dhidi ya JamaicaPicha: Getty Images/Elsa

Kocha wa England Phil Neville  amesema  baada  ya  mchezo huo kwamba  timu  yake  haiwezi kumudu kuthubutu  kupoteza kasi ya mchezo  wake , na  inapaswa  kucheza  kwa  ukakamavu  ule  ule  na kumiliki  mpira iwapo  inataka  kusonga  mbele  katika  kombe  la dunia  la  wanawake.

Ante Milicic ana  siku  nne  kuweza  kuipa uhai  timu  yake  ya wanawake  wa  Australia  katika  kampeni  ya  kombe  la  dunia baada  ya  kushindwa  na  Italia  na  hakuna  kitakachopuuzwa  kabla ya  kukabiliana  na  Brazil  mjini  Montpellier  siku  ya  Alhamis.

Fussball  FIFA Frauen WM Australien - Italien
Ni patashika kati ya wachezaji wa Australia wakipambana na wachezaji wa Australia katika kombe la dunia la wanawakePicha: picture-alliance/AP Photo/F. Seco

Australia  kwa  jina  la  utani  Matildas, walishangazwa  kwa  bao  la dakika  za  mwisho  la  barbara Bonansea kwa  kichwa  jana, na kuipa Italia, Squadra Azzurre  kwa  mabao 2-1  katika  kundi  C.

Astralia  itapambana  na  Brazil , ambayo  ilifungua  kampeni  yake kwa  ushindi  wa  mabao 3-0 dhidi  ya  Jamaica na  kujihakikishia nafasi  nzuri  kuelekea  katika  timu  16 zitakazoingia  katika  duru  ya mtoano.