1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

FIFA Conf. Cup Ujerumani kuumana na Chile

Sekione Kitojo
2 Julai 2017

Michuano ya kombe la mabingwa wa mabara maarufu kama Confederation Cup inafikia  kilele leo Jumapili (02.07.2017)wakati mabingwa wa kombe la dunia mwaka 2014 Ujerumani inapambana na Chile mabingwa wa Amerika kusini.

https://p.dw.com/p/2fmEq
BG Confed Cup 2017 | Team Deutschland
Picha: picture alliance/dpa/C. Kolbert

Urusi imesifiwa jana Jumamosi kwa  kufanikisha  kwa  mafanikio mashindano  hayo ya  kombe  la  mabara , ikiwa  ni  kujipasha  moto kwa  ajili  ya  fainali  za  kombe  la  dunia , licha  ya  kwamba nchi hiyo  imekabiliwa na  maswali  mapya  juu  ya suala  la  matumizi  ya madawa  ya  kuongeza  nguvu  misuli, yaani  doping.

Nahodha  wa Ujerumani  Julian Draxler alijiunga  na  rais  wa shirikisho  la  kandanda  duniani  FIFA Gianni Infantino katika kuishukuru Urusi  kabla ya  fainali  ya  leo. "Ahsante  kwa maandalizi yenu  mazuri, kwa  kuwa na  watu wengi  wa  usaidizi  wakati  wote wa  mashindano, na   kwa  kila  wakati  ambapo  mmetufanya tujisikie salama," Draxler  amesema  katika  taarifa  iliyochapishwa Jumamosi  na  timu  ya  Ujerumani.

BG Confed Cup 2017 | Chile Aranguiz und Vidal
Wachezaji wa Chile wakishangiria bao katika michuano ya kombe la mabara nchini Urusi Picha: Getty Images/AFP/R. Arangua

Infantino  alisema  baadaye  katika  mkutano  na  waandishi  habari katika  uwanja  wa  mpira  wa  mjini  St.Petersburg  kwamba "kila  kitu kilienda  vizuri,"  Urusi. Tulikuwa  tunasikia  kuhusiana na ghasia , kuhusu  matukio, kuhusu  wahuni  michezoni , kuhusu ubaguzi, lakini hatukuwa  na kitu chochote," Infantino  alisema, akimaanisha maswali  ya  kabla  ya  michezo hiyo  ambayo  yalihusishwa  na kandanda  katika  taifa  hilo  mwenyeji.

Fußball Confederations Cup 2017 Deutschland - Mexiko
Julian Draxler nahodha wa timu ya taifa ya Ujerumani katika kombe la mabara nchini UrusiPicha: Getty Images/Bongarts/A. Hassenstein

Pamoja  na  hayo  kivuli  cha  doping kilichoko katika  michezo  nchini Urusi  kutokana  na  wimbi  la  ripoti  za  shirika  linalopambana  na matumizi  ya  madawa  hayo  katika  michezo duniani  tangu  mwaka 2015 pia  zimejitokeza  wakati  wa  michuano  hiyo  ya  kupasha mwili  joto  ya  wiki  mbili  kabla  ya  kombe  la  dunia.

Urusi  na  doping

FIFA  inafahamu  kuhusu  sampuli  155  za  watuhumiwa zilizotolewa na  wachezaji  nchini  Urusi  ambazo  zinahitaji  kufanyiwa  uchunguzi, mtaalamu  wa  WADA  aliyeteuliwa  kuchunguza Richard McLaren amekiambia  kitu  cha  televisheni  nchini  Ujerumani  ARD.

Deutschland Fußball Nationalmannschaft | Mannschaftsfoto
Kikosi cha timu ya taifa ya Ujerumani Die Mannschaft kinachoshiriki kombe la mabara nchini UrusiPicha: picture-alliance/GES/M. Gilliar

Infantino , ambaye  aliongozana  na  naibu  waziri  mkuu  wa  Urusi Vitaly Mutko, alisema  jana  Jumamosi  hawezi  kupanga  muda maalum kwa  kesi  hizo  za  Urusi  ambazo  kamati  ya  nidhamu  ya FIFA inapaswa  kutekeleza  kutokana  na  ripoti za  McLaren.

Hata  hivyo, maamuzi  muhimu  kuhusiana  na  madai  ya  profesa huyo  kutoka  Canada  wa  masuala  ya  sheria  dhidi  ya  Urusi yanakaribia  na  yanaweza  kutangazwa  katika  muda  wa  wiki chache zijazo.

Russland FIFA Präsident Gianni Infantino - FIFA Confederations Cup Russia 2017
Rais wa FIFA Giovanni InfantinoPicha: Getty Images/M. Hangst

Jopo  la  kimataifa  la  kamati  ya  Olimpiki  inajitayarisha  kutangaza matokeo ya  hukumu  yake  ya  mwanzo  inayohusu  wanamichezo wa  Urusi  katika  michezo ya  majira  ya  baridi  mwaka  2014 ambao  wanashukiwa  kunufaika  na  njama  za  doping zilizoungwa na  serikali  katika  maabara  ya  Olimpiki  mjini  Sochi.

"Tunasubiri  pia ripoti  hizo," Infantino  alikiri  Jumamosi. Mutko, ambaye  ni  mwenyekiti  wa  kamati  ya  maandalizi ya  kombe  la dunia  mwaka  2018 na  alihusishwa  katika  ushahidi  wa  McLaren kuficha kesi  moja  ya  doping  katika  kandanda, kwa  mara  nyingine tena  alikanusha  vikali  madai  kwamba  serikali  ilikuwa  inaendesha mpango  huo  wa  doping.

Fußball FIFA Confederations Cup Putin und Infantino
Rais wa Urusi Vladimir Putin (kulia) akiwa pamoja na rais wa FIFA Gianni Infantino (kushoto)Picha: picture-alliance/dpa/D. Astakhov

Rais  wa  Urusi  Vladmir  Putin  hana  mpango  wa  kuhudhuria  fainali ya  kombe  la  mabara  leo  mjini  St.Petersburg zimeeleza  duru  za FIFA. Putin alihudhuria  mchezo  wa  ufunguzi  wa  mashindano  hayo mjini  St. Petersburg  hapo  Juni 17  wakati  aliposhuhudia  mchezo kati  ya  Urusi  na  New zealand akiwa  pamoja  na  rais  wa  FIFA Giovanni Infanitino.

Mwandishi: Sekione  Kitojo / dpae / ape

Mhariri: Sylvia  Mwehozi