1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Fujimori ameadhibiwa kufungwa jela miaka sita

12 Desemba 2007
https://p.dw.com/p/CaSQ

LIMA:

Rais wa zamani wa Peru,Alberto Fujimori ameadhibiwa kifungo cha miaka sita kwa hatia ya matumizi mabaya ya mamlaka.Mahakama katika mji mkuu Lima,imesema Fujimori alipokuwa madarakani, alitoa amri ya kusaka nyumba ya wakili mmoja bila ya kibali.

Fujimori mwenye umri wa miaka 69 anakabiliwa pia na mashtaka ya mauaji,ukiukaji wa haki za binadamu na rushwa.Yeye alitawala nchini Peru kuanzia mwaka 1990 hadi 2000 na alikimbilia Japan serikali yake ilipoanguka.