1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Gaddafi apinga kutambuliwa kwa Baraza la Mpito la Waasi wa Libya

Mnette,Sudi/dpae16 Julai 2011

Kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi amepinga hatua iliyochukuliwa na kundi la nchi na taasisi za kimataifa 40, kulitambua Baraza la Mpito la Waasi wa Libya kama chombo halali kinachowakilisha wananchi wa Libya.

https://p.dw.com/p/RaCv
This video image taken from Turkish television Libyan leader Moammar Gadhafi is seen during an interview with the TV channel TRT, in Tripoli, Libya, Tuesday March 8, 2011. Gadhafi said in an interview broadcast Wednesday that Libyans would fight back if Western nations impose a no-fly zone to prevent the regime from using its air force to bomb government opponents staging a rebellion. (AP Photo/TRT)
Kiongozi wa Libya, Muammar GaddafiPicha: AP

Kundi hilo la mashauriano kuhusu Libya, lilikutana jana mjini Istanbul Uturuki. Katika mkutano huo, lilitangaza kutambuliwa kwa baraza la waasi kama mwakilishi wa watu wa Libya na " serikali yenye mamlaka". Marekani imeungana na mataifa mengine makuu kuwatambua waasi wa Libya kama chombo halali cha uongozi nchini Libya.