1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Gbagbo haendi kokote

Martin,Prema6 Aprili 2011

Laurent Gbagbo anangángánia urais nchini Cote d´Ivoire, licha ya kushinikizwa kumkabidhi madaraka hasimu wake Alassane Ouattara, anaetambuliwa na jamii ya kimataifa kama rais halali wa Cote d´Ivoire.

https://p.dw.com/p/RFio
Ivory Coast, President Laurent Gbagbo, Smile during an exclusive interview at his residence, in Abidjan, Sunday, Dec. 26, 2010. West African leaders are giving the man who refuses to leave Ivory Coast's presidency a final chance to hand over power and are threatening to remove him by force if needed, though doubts exist about whether the operation could be carried out. (AP Photo/Sunday Alamba)
Rais wa Cote d´Ivoire Laurent GbagboPicha: AP

Katika mahojiano yake ya simu na kituo kimoja cha televisheni cha Ufaransa, Laurent Gbagbo amekataa kumtambua Ouattara,mshindi wa uchaguzi wa rais uliofanyika Novemba mwaka jana nchini humo.

ABIDJAN, April 5, 2011 (Xinhua) -- A French military helicopter patrols above Abidjan, Cote d'Ivoire, April 1, 2011. The United Nations Operation in Cote d'Ivoire (UNOCI) and the French force undertook a military operation against forces loyal to the incumbent Ivorian leader Laurent Gbagbo on April 4. (Xinhua/Ding Haitao)(lyx) XINHUA /LANDOV
Helikopta ya jeshi la Ufaransa ikipiga doria AbidjanPicha: picture-alliance/dpa

Gbagbo ametazamiwa kuondoka madarakani, baada ya viongozi wake wa kijeshi, kusalim amri hiyo jana, baada ya kushambuliwa vikali na wafuasi wa Ouattara waliosaidiwa na vikosi vya Ufaransa na Umoja wa Mataifa mjini Abidjan.

Kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa Mataifa, Laurent Gbagbo amejificha katika kasri la rais mjini Abidjan.