1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hali ya wasiwasi yawakabili Wakenya huku Onyancha akifikishwa mahakamani

Josephat Nyiro Charo15 Juni 2010

Mshukiwa huyo anadai aliwaua watu 19 lakini alitaka kuua 100

https://p.dw.com/p/NrXe

Phillip Onyancha mwenye umri wa miaka 32, amefikishwa mahakamani hii leo kwa mauaji ya Anthony Njirua Muiruri. Polisi wanasema walimkamata jamaa huyo kwa kumteka nyara kijana huyo Muiruri, kwa kumfuatilia kupitia simu yake ya mkononi ambayo alikuwa akiitumia kuwashinikiza wazazi wake wamlipe fedha kabla kumuachilia. Polisi pia wanasema Onyancha amekiri alimua kijana huyo pamoja na watu wengine 18.

Akiwa mahakamani hii leo, Onyancha hakujibu mashitaka yanayomkabili kwa sababu hakuwa na wakili.

Habari za kutisha kuhusu jamaa huyo ambaye amejitokeza hadharani kukiri kwamba amekuwa akitekeleza mauaji ya kikatili, na kisha kunywa damu za watu hao, zinazidi kuzusha hofu kote nchini Kenya.

Sasa visa vya kupotea watu vimeanza kuhusishwa moja kwa moja na ukatili huo unaohofiwa umetekelezwa na wafuasi wa makundi yenye itikadi kali wanaotaka kumaliza kiu chao kwa kunywa damu ya wanadamu.

Mwandishi wetu Eric Ponda kutoka Mombasa ametuandalia taarifa ifuatayo.