1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hujuma katika timu ya Mercedes F1?

2 Mei 2016

Dereva Nico Rosberg anaendelea kupata ushindi na Lewis Hamilton akikumbwa na matatizo licha ya kumaliza katika nafasi ya pili katika mashindano ya Jumapili ya Russian Grand Prix

https://p.dw.com/p/1Igaj
Russland Formel 1 in Sotschi - Siegerehrung
Picha: Reuters/M. Shemetov

Rosberg alipata ushindi wake wa saba mfululizo na kuutanua uongozi wake wa ubingwa wa dunia kwa pengo la pointi 43. Muingereza Hamilton aliendelea kukumbwa na hitilafu za kimitambo na hajashinda mashindano yoyote msimu huu tangu aliposhinda taji la ulimwengu Oktoba 2015.

Mercedes imepuuza madai kuwa wanampendelea Mjerumani Rosberg kumliko Hamilton msimu huu. Mkuu wa timu ya Mercedes Toto Wolff alisisitiza kuwa hawawezi kamwe kumhujumu Hamilton. Kimi Raikkonen wa Ferrari alimaliza wa tatu katika mashindano hayo ya Sochi nchini Urusi.

Mwandishi: Bruce Amani/AFP/DPA
Mhariri: Yusuf Saumu