1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mawaziri wa mambo ya kigeni wa umoja wa Ulaya wakutana Luxemburg.

Kitojo, Sekione16 Juni 2008
https://p.dw.com/p/EKSS
Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani Steinmeier ambaye ametoa ushauri wa kuiacha Ireland kando katika mchakato wa kuleta ujumuisho katika umoja wa Ulaya kutokana na nchi hiyo kuukataa mkataba wa Lisbon.Picha: AP



Tatizo   linalohusu  mkataba  wa  Lisbon  linapaswa kwanza  kushughulikiwa,  na    wahusika  katika umoja  wa  Ulaya. Hali  itakuwaje  ili  kusonga mbele. Leo  hii  mawaziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa umoja  wa  Ulaya  watalizungumzia  suala  hilo. Waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Ujerumani  Frank-Walter  Steinmeier tayari  ameliweka  suala  la  kura ya  maoni  iliyofanyika    hivi  karibuni  nchini  Ireland kuwa  moja  kati  ya  mada  katika  mkutano  wa umoja  huo.



Waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Ujerumani  Frank-Walter  Steinmeier  anadiriki  kuwa   mtu  wa  kwanza kutoa pendekezo   ambalo  si  rahisi , kwamba  umoja wa  Ulaya  unaweza  kufanyakazi  bila  ya  Ireland. Kura  ya  hapana  iliyopigwa  na  wapigakuwa  wa Ireland , kwa  mara  nyingine  tena  kundi  hilo  la mataifa  wanachama  27  limeingia  katika  mzozo mwingine  mkubwa, na  mawaziri  wa  mambo  ya kigeni , wameingia  katika  kazi  ya  kutafuta  njia  ya kujitoa. Waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Ujerumani Frank-Walter  Steinmeire  amesema  kuwa,

pamoja  na  hayo  , inawezekana, kuwa  Ireland ilikuwa  inajitafutia  njia  kwa  muda  mrefu  kujitoa katika   umoja  wa  Ulaya,  pamoja  na  kujitoa  katika uboreshaji   wa  hatua  za  ujumuisho , na   sasa wanapaswa  kukaa  kando  ili  tuweze  kuuimarisha mkataba  wa  Lisbon  kwa  kupitia  mataifa  26 yaliyobaki.

Waziri  huyo  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Ujerumani anataka  mpango  wake  huo upatiwe  muda  wa kuangaliwa  na  wenzake  katika  mkutano  wao  mjini Luxemburg,  na  iwapo  yeye  pamoja  na  wenzake wanaweza  kulipima  hilo, inawezekana   kuwa ni suala  lenye  shaka shaka. Ufaransa, Poland  na Uingereza  tayari  wametoa  ishara,   ya  kuwa  na hofu  kuwa  mataifa  mengine  yanaweza  kuutupa mkataba  huo  kando  kwa  kura  ya  hapana  pia.

Kura  ya  pili  ya  hapana  inaweza  kuuingiza mkataba  huo  wa  Lisbon   katika   matatizo  zaidi, na  kuukwamisha  kabisa, na  hali  hiyo serikali  ya Uingereza  inataka  iepukwe,  kutokana   na  kwamba toka  hapo  Uingereza  ilikwisha  toa vipengee  kadha vya  kujifaidia  katika  mkataba  huo.


Kuidhinishwa  kwa  mkataba  huo  wa  mageuzi katika  kila  nchi  kutaendelea, hilo  ni  moja. Kura  ya hapana   ya  Ireland   ni  kama   chombo  kilicholeta somo  na  kujitambua,  kwa  umoja  huo. Ndio sababu  leo  mchana  inawezekana  pia  ujumbe wote  wa  Ireland  kuwajibika  zaidi. Ni  kitu   gani mataifa  ya  Ulaya  yameweza   kupata  mwanga  wa matumaini, ni  suala  ambalo  liko  mikononi  mwa viongozi  wa  mataifa  ya  Ulaya  waliokutana  mjini Luxemburg  kama  anavyosema  kiongozi  wa Luxemburg  Jean-Claude Juncker.

Tunapaswa  kujiingiza  katika  mazungumzo  ya maana   kutokana  na  kura  hiyo  ya  hapana  ya Ireland  kutuhusu  sisi. Na  baadaye  tutaona , vipi tunaweza  kujitoa  katika  hali  hii  ambayo  si  nzuri.

Tunaamini  kuwa  tunaweza  kuendelea  na  utaratibu wetu  na  kuchukua  pendekezo  la  Ireland  ama majadiliano  mengine  hapo  baadaye.

Kama  walivyo  mawaziri  wa  mambo  ya  kigeni , baadaye   wiki  hii  viongozi  wa  serikali   watakuwa na  majadiliano  kuhusiana  na  kura  hiyo  ya hapana  iliyopigwa  na  wapigakura  wa  Ireland na mada  ni  kuwa  watafanya  nini  kusonga  mbele, swali  hilo  litasubiri  hadi , hadi  pale  mataifa  hayo ya  umoja  wa  Ulaya  yatakapoweza  kujitoa  katika mzozo  huo  mpya.

►◄