1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

JAKARTA: Irak imeifunga Saudi Arabia

29 Julai 2007
https://p.dw.com/p/CBdx

Irak imeshinda Kombe la Asia,baada ya kuikandika Saudi Arabia mkwaju mmoja kwa bila katika fainali iliyochezwa mji mkuu wa Indonesia,Jakarta.

Hapo kabla,kocha wa Irak,Jorvan Viera alisisitiza umuhimu wa mchezo huu kwa wachezaji wake na nchi yao katika wakati huu wa ghasia za kisiasa nchini Irak.Alisema:

„Huenda ikawa wataweza kuyakaweka kando matatizo ili waweze kucheza mpira na kuwafurahisha wenzao nyumbani na kuwapatia sababu ya kutabasamu.“