1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

JERUSALEM: Ehud Olmert amehojiwa kuhusu vita vya Lebanon

1 Februari 2007
https://p.dw.com/p/CCW6
Mjumbe wa Umoja wa Mataifa Ibrahim Gambari akiwa na kiongozi wa upinzani alioko kizuizini Aung San Suu Kyi wakati alipotembelea Myanmar hivi karibuni.
Mjumbe wa Umoja wa Mataifa Ibrahim Gambari akiwa na kiongozi wa upinzani alioko kizuizini Aung San Suu Kyi wakati alipotembelea Myanmar hivi karibuni.Picha: AP

Waziri mkuu wa Israel,Ehud Olmert ameanza kutoa ushahidi wake mbele ya tume maalum ya serikali, iliyoundwa kuchunguza vita vya mwaka jana kati ya Israel na wanamgambo wa Hezbollah nchini Lebanon. Viongozi wa serikali na wakuu wa majeshi, walilaumiwa vikali jinsi walivyoendesha vita hivyo vya mwezi mmoja.Waziri mkuu Olmert ni wa mwisho kutoka jumla ya mashahidi 70 waliohojiwa mbele ya tume ya uchunguzi,inayotazamiwa kutoa ripoti yake ya kwanza kati kati ya mwezi wa Machi.