1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

JERUSALEM: Israel yaonya kuchukua hatua kali zaidi

20 Mei 2007
https://p.dw.com/p/CC0F

Waziri mkuu wa Israel,Ehud Olmert ametishia kuchukua hatua kali zaidi za kijeshi katika Ukanda wa Gaza ikiwa kundi la Hamas halitoacha

kurusha makombora kusini mwa Israel.Mashambulio ya angani ya Israel hii leo yameua Wapalestina 3 walioshukiwa kuwa wanamgambo wa Hamas.Kama Wapalestina 21 wameua katika mashambulio ya siku tano yaliofanywa na ndege na vifaru vya Israel.