1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

John Kerry kuzuru mashariki ya kati na Afrika

18 Mei 2013

Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani John Kerry anatarajiwa kusafiri kwenda katika mataifa ya mashariki ya kati na Afrika kuanzia Jumanne ijayo kwa ziara itakayomchukua hadi Mei 27.

https://p.dw.com/p/18aEs
US Secretary of State John Kerry exits his government aircraft (Foto: Reuters) / Eingestellt von wa
Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani John KerryPicha: Reuters

Kerry  anatarajiwa  kuanza ziara  yake  mjini  Muscat  siku ya  Jumanne (21.05.2013), ikifuatiwa  na  Jordan  siku  ya  Jumatano, ambako atakutana  na  kile  kinachoitwa  "washirika  muhimu  wa  kimataifa", kuangalia uwezekano  wa  kupatikana  kwa  suluhisho  la  kisiasa kupitia  majadiliano  nchini  Syria , wizara  ya  mambo  ya  kigeni nchini  Marekani  imesema  katika  taarifa.

Mkutano  huo  unakuja  kabla  ya  mkutano  mkubwa  wa  kimataifa kuhusu  Syria unaopangwa  na  Urusi  na  Marekani , na  ambao unatarajiwa  kufanyika  mwezi  ujao.

Russian President Vladimir Putin (R) and the US Secretary of State John Kerry (L) hold talks in the Kremlin in Moscow on May 7, 2013. Kerry sought today to narrow differences over the conflict in Syria with Putin, urging the Russian strongman to find common ground to help end the bloodshed. AFP PHOTO/POOL/MLADEN ANTONOV (Photo credit should read MLADEN ANTONOV/AFP/Getty Images)
Kerry akiwa katika majadiliano na rais Putin wa UrusiPicha: MLADEN ANTONOV/AFP/Getty Images

Siku  ya  Alhamis  na  Ijumaa , Kerry anatarajiwa  kuzuru  Jerusalem na  Ramallah  kufuatilia  mazungumzo  juu  ya  kuleta  pamoja  Israel na  Palestina  katika  meza  ya  majadiliano, kujadili amani, taarifa hiyo  imesema.

Sherehe za Umoja wa  Afrika

Pia  siku  ya  Ijumaa , Kerry  anatarajiwa  kusafiri  kwenda  mjini Addis Ababa kushiriki  katika  sherehe  za  siku  mbili  za kuadhimisha  miaka  50  tangu  kuundwa  kwa  Umoja  wa  nchi  za Afrika  OAU, ambao  hivi  sasa   unajulikana  kama  Umoja  wa Afrika, AU. viongozi  kutoka  sehemu  mbali  mbali  za  Afrika watahudhuria  sherehe  hizo.

Hapo  Mei 26 , waziri  Kerry  anapanga  kurejea  mjini  Amman Jordan  kushiriki  katika  jukwaa  la  kiuchumi  la    dunia.

Wakati  huo huo  baraza  la  usalama  la  umoja  wa  mataifa  linatafakari ombi kutoka  kwa  maafisa  wa  ngazi  ya  juu  wa  shirika  la  misaada  la umoja  huo  linalodai  kufikishwa  kwa  misaada  katika  nchi iliyoharibiwa  kwa  vita  ya  syria, hatua  ambayo  inaweza kusababisha  hali  ya  mivutano  baina  ya  Urusi  na  mataifa  ya magharibi  kuhusiana  na  upelekaji  wa  misaada  ya  kiutu  kupitia mipakani, wamesema  wanadiplomasia  wa  Umoja  wa  Mataifa.

Members of the United Nations Security Council listen to Syria's U.N. Ambassador Bashar Ja'afari during a Security Council meeting on the situation in Syria at United Nations headquarters Thursday, July 19, 2012. Russia and China vetoed a U.N. resolution to imposes non-military sanctions on Syria. (AP Photo/Kathy Willens)
Baraza la usalama la umoja wa mataifaPicha: dapd

Wakimbizi wamiminika  nchi jirani

Wakati nchi  jirani  za  Jordan, Lebanon, Uturuki  na  Iraq zinasumbuka    kuhimili  wimbi  la  wakimbizi  wanaoingia  katika  nchi zao , ambao  shirika  la  Umoja  wa  Mataifa  la  kuwahudumia wakimbizi UNHCR, limesema  siku  ya  Ijumaa, (17.05.2013), imevuka  idadi  ya  watu  milioni  1.5, maafisa  wa  umoja huo wameliambia  baraza  la  usalama , kuwa  kuna  mamilioni  ya  watu wanaohitaji  misaada  ndani  ya  Syria.

Lakini  mpambano  wa  aina  hiyo  kuhusiana  na  azimio  jipya katika  baraza  hilo  lenye  wajumbe  15, ambalo  kwa  muda  mrefu limeendelea  kukwama  kuhusiana  na  vipi  wanaweza kuushughulikia  mzozo  wa  Syria  uliodumu  miaka  miwili  sasa, huenda  likaachwa  hadi  baada  ya  mkutano  wa  kimataifa  kuhusu Syria  utakaofanyika  mjini  geneva  mwezi  ujao, wameeleza wanadiplomasia  wa  Umoja  wa  Mataifa.

Syria's President Bashar al-Assad speaks at the Opera House in Damascus in this still image taken from video January 6, 2013. REUTERS/Syrian TV via Reuters TV (SYRIA - Tags: POLITICS PROFILE TPX IMAGES OF THE DAY) NO SALES. NO ARCHIVES. FOR EDITORIAL USE ONLY. NOT FOR SALE FOR MARKETING OR ADVERTISING CAMPAIGNS. THIS IMAGE HAS BEEN SUPPLIED BY A THIRD PARTY. IT IS DISTRIBUTED, EXACTLY AS RECEIVED BY REUTERS, AS A SERVICE TO CLIENTS. SYRIA OUT. NO COMMERCIAL OR EDITORIAL SALES IN SYRIA
Bashar al-Assad akihutubia kwa njia ya TelevisheniPicha: Reuters

Urusi, mshirika  wa  karibu  wa  rais  wa  Syria  Bashar al-Assad   na China  zimetumia  kura  ya  turufu  mata  tatu  kuzuwia  baraza  hilo kuchukua  hatua  dhidi  ya  Assad, hatua  zilizoungwa  mkono  na mataifa  mengine  matatu  yenye  kura  hiyo, Marekani, Ufaransa  na Uingereza.

Viongozi  wa  mataifa  ya  magharibi  wamechukua   tahadhari kuhusu  uwezekano  wa  mafanikio  ya  mkutano  wa  syria  mjini Geneva  kuwa  unaweza  kupata  kufikia  kuondoa  mkwamo, na mapendekezo   ya  Urusi   kuwa  Iran  ni  lazima  ihudhurie  katika mazungumzo  hayo  yameanza  kufanya  mambo  kuwa  magumu.

Mwandishi : Sekione  Kitojo / rtre / dpae

Mhariri: Caro Robi