1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KABUL: Hakuna maendeleo kuhusu mateka wa Korea

29 Julai 2007
https://p.dw.com/p/CBe8

Maafisa wa Afghanistan wamesema,hakuna maendeleo yaliyopatikana katika majadiliano yake pamoja na wazee wa makundi ya kikabila kuhusu hatima ya mateka 22 wa Korea ya Kusini wanaozuiliwa na wanamgambo wa Taliban.Wateka nyara wametishia kuwauwa mateka hao,ikiwa serikali haitowaachilia huru wafungwa kadhaa wa Kitaliban walio jela. Mateka hao wa Korea ya Kusini walikamatwa zaidi ya juma moja lililopita.Mmoja wao ameshauliwa na wanamgambo.