KABUL: Operesheni mpya ya kijeshi dhidi ya Taliban
3 Juni 2007Matangazo
Wanajeshi wa Afghanistan wakisaidiwa na majeshi ya madola shirika ya kigeni,wameanzisha operesheni mpya ya kijeshi dhidi ya wanamgambo wa Taliban.Kwa mujibu wa wizara ya ulinzi ya Afghanistan,azma ya operesheni hiyo ni kurejesha hali ya usalama kusini mwa nchi.Wakati huo huo msemaji wa wanamgambo ametishia kuwa kutafanywa mashambulizi mapya.