1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KABUL: Waafghanistan wanane wauwawa katika shambulio la majeshi ya NATO

18 Oktoba 2006
https://p.dw.com/p/CD1Z

Shambulio la angani la jeshi la NATO limewaua raia takriban wanane wa Afghanistan katika mkoa wa Kandahar kusini mwa nchi hiyo. Raia wengine tisa wamejeruhiwa katika hujuma hiyo.

Gavana wa mkoa wa Kandahar, Asadullah Khalid, amesema vifo hivyo vimesababishwa na mabomu ya NATO yaliyoyapiga makaazi matatu katika wilaya ya Zhari mkoani humo.

Shirika la NATO limesema linajutia vifo vya raia hao na linafanya kila juhudi kupunguza uwezekano wa kutokea maafa wakati wa operesheni zake.