1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kenya yatambulisha kikosi cha Olimpiki Tokyo

Bruce Amani
21 Juni 2021

Kenya imekitambulisha kikosi chake kitakachoshiriki katika Michezo ya Olimpiki ya Tokyo kikiwa na orodha ya Zaidi ya wanariadha 40 wakiwemo. Wanariadha Timothy Cheruiyot na Conseslus Kipruto hawakufuzu

https://p.dw.com/p/3vHwp
Leichtathletik-WM Doha 2019 Frauen Finale 5000 Konstanze Klosterhalfen
Picha: Reuters/A. Szmigiel

Kenya imekitambulisha kikosi chake kitakachoshiriki katika Michezo ya Olimpiki ya Tokyo kikiwa na orodha ya Zaidi ya wanariadha 40 wakiwemo bingwa wa dunia Hellen Obiri na mshindi wa dhahabu katika Olimpiki ambaye ni bingwa mtetezi wa mbio za mita 1,500 Faith Chepngetich.

Majina maarufu yaliyoachwa nje ni bingwa wa ulimwengu wa mita 1,500 kwa wanaume Timothy Cheruiyot na bingwa mtetezi wa Olimpiki katika mbio za mita 3,000 kuruka viunzi na maji Conseslus Kipruto baada ya wote kushindwa katika mbio za mchujo.

Timu hiyo pia inawajumuisha wanariadha Eliu Kipchoge, Brigid Kosgei na Geoffrey Kamworor ambaye atashiriki mbio za mita 10,000. TeamKenya inapanga kelekea Japan Julai 5 kwa ajili ya kuweka kambi mjini Kurume kwa ajili ya Michezo hiyo itakayoanza Julai 23.

AP/Reuters