1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kigali:Mkutano wa wanawake barani Afrika

22 Februari 2007
https://p.dw.com/p/CCPk

Mkutano wa wanawake barani Afrika unaanza leo katika mji mkuu wa Rwanda-Kigali.Rwanda ni nchi inayoongoza duniani kwa kuwa na idadi kubwa ya wabunge wanawake duniani wakiwa karibu nusu ya wabunge wa nchi hiyo.

Mkutano huo utafunguliwa na Rais wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf ambaye amealikwa kuwa mgeni Rasmi. Rais Sirleaf ni Rais wa kwanza mwanamke barani Afrika, na kuchaguliwa kwake kuiongoza Liberia, kumegeuka mfano katika juhudi za kupigania usawa wa jinsi na ukombozi mwa wanawake barani humo.