1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

220711 Äthiopien Hunger

25 Julai 2011

Ukame mbaya umelikumba eneo la Pembe ya Afrika na kusababisha tishio kubwa la njaa pia nchini Ethiopia. Wakati huo huo juhudi za kuyaokoa maisha ya mamilioni ya watu zitaimarishwa kwenye kikao cha FAO.

https://p.dw.com/p/122oh
Nembo ya Shirika la FAO

Wajumbe  wa  serikali, wawakilishi wa Umoja  wa  Mataifa na wa mashirika  ya  misaada leo wanakutana mjini Rome  kwa ajili ya kikao cha dharura kulijadili baa la njaa kwenye eneo la Pembe ya Afrika. Wajumbe  kwenye  kikao hicho wanazungumzia njia za kuwasaidia watu wapatao milioni 12 waliomo katika hatari ya kufa njaa.

Kikao  hicho kinafanyika kufuatia  shinikizo  la  kimataifa  kuwataka viongozi  wa dunia waongeze  misaada  kwa  ajili  ya mamilioni  ya watu wanaotishiwa  na baa  la  njaa  lilisosababishwa na ukame mbaya ambao haujawahi kuonekana katika  historia ya miaka 60 iliyopita katika eneo  la Pembe ya  Afrika.

Flash-Galerie Dürre ohne Ende Hunger und Dürre in Äthiopien
Ukame uliokithiri: Mifugo yafa kwa wingi na njaa imesambaa EthiopiaPicha: picture-alliance/dpa

Vifo vimekuwa vingi

Kwa mujibu  wa  taarifa za maafisa   wa  Umoja  wa  Mataifa  njaa imeshawaua  maalfu ya  watu  katika  sehemu hiyo .

Katibu Mkuu  wa  Umoja  wa Mataifa Ban - Kimoon  ametoa  mwito kwa wafadhili wa kuchangisha kiasi  cha dola Bilioni 1.6 kwa ajili  ya sehemu mbili  za  kusini mwa  Somalia  zilizotangazwa na  Umoja wa Mataifa wiki iliyopita kuwa sehemu zenye  maafa  ya njaa.

Shirika la  Chakula  na Kilimo la Umoja  wa  Mataifa lililouandaa mkutano  huo wa mjini  Rome  leo  limetahadharisha  kwamba  hali itazidi  kuwa  ya maafa   makubwa  ikiwa  hatua hazitachukuliwa.

Nchi zilizokumbwa na  athari  za ukame   kwenye  pembe  ya Afrika ni pamoja  na Kenya, Uganda,Sudan,  Djibouti na  Ethiopia.

Mratibu  wa misaada wa Umoja wa  Mataifa Valerie Amos ameitembelea  Somalia na kujionea   mwenyewe jinsi  hali  ilivyo.

Akizungumza na waandishi  habari mjini   Addis Ababa alieleza kuwa,

"Sasa  hivi  natokea kwenye  jimbo la Somalia.Huko niliweza kuzungumza  na  wanawake  waliotembea pamoja na watoto wao kwa  muda  wa saa tano  wakitafuta chakula  na huduma  za afya.Watoto  zaidi  na  zaidi  wanasibika na utapiamlo. Wafugaji wameipoteza mifugo yao na  hivyo wamepoteza njia za kujiendeshea  maisha."

Hungersnot in Somalia Afrika
Wanawake wa Kisomali wakisubiri chakula cha msaada MogadishuPicha: dapd

Utapia mlo na njaa

Nchini  Ethiopia  watu milioni  nane yaani  asilimia  10 ya  wananchi wanasibika na utapiamlo. Licha ya  juhudi  za serikali ya  Ehtiopia kuongeza vitega uchumi  katika sekta  ya kilimo  bado hali  haijawa nzuri sana. Pamoja na hayo sera  ya kuwakodisha ardhi wakulima kutoka nje ya nchi inazidi kukosolewa.Kutokana an hali hiyo Ethiopia inayojiita kuwa chui milia  wa Afrika bado inaandamwa na  gamba  la njaa.

Weltkarte Hunger herausgegeben von der FAO Datenmaterial 1994-96
Ramani inayoionyesha hali ya chakula ulimwenguniPicha: FAO

Mwaka  jana Waziri Mkuu  wa  Ethiopia Meles  Zenawi  alisema miongoni mwa  malengo ya mpango wa  maendeleo wa  maika mitano ni kujitosheleza  kwa  mahitaji ya chakula  sambamba  na kuzalisha  cha ziada kwa  ajili ya kuuza nchi  za nje. Lakini  hali halisi ni nyingine  kwa  Ethiopia mnamo mwezi  wa  februari  WaziriMkuu Zenawi alilazimika kuomba  msaada wa  chakula  kutoka  kwa shirika  la chakula duniani  WFP kwa ajili  ya  wananchi wake milioni tatu waliokuwa  wanatishiwa  na  njaa .

Mwandishi/Schadomsky ,Ludger - Mtullya  Abdu

Mhariri/ Abdul-Rahman, Mohamed