1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Korea ya Kaskazini yafunga virago

P.Martin/ZPR/AFPE22 Juni 2010

Michuano ya kuwania Kombe la Dunia ikiendelea nchini Afrika Kusini,Chile na Ureno zimeashiria kujongelea duru ya pili ya michuano hiyo.

https://p.dw.com/p/NzdR
epa02214367 Portugal's Cristiano Ronaldo balances the ball in his neck before scoring the 6-0 lead during the FIFA World Cup 2010 group G preliminary round match between Portugal and North Korea at the Green Point stadium in Cape Town, South Africa, 21 June 2010. EPA/HELMUT FOHRINGER Please refer to www.epa.eu/downloads/FIFA-WorldCup2010-Terms-and-Conditions.pdf EPA +++(c) dpa - Bildfunk+++
Cristiano Ronaldo wa Ureno kabla ya kuikandika Korea ya Kaskazini bao la sita uwanajani Green Point mjini Cape Town, Afrika Kusini.Picha: AP

Katika mchezo wa jana Jumatatu, Chile iliifunga Uswisi kwa bao 1-0 na Ureno nayo imeitoa Korea ya Kaskazini katika kinyanganyiro hicho cha Kombe la Dunia baada ya kuikandika mabao 7-0.

Katika mechi nyingine,bingwa wa Ulaya Uhispania, hatimae imefanikiwa kupata ushindi wake wa kwanza katika michuano hiyo ya Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini baada ya kuifunga Honduras mabao 2-0.

epa02215109 Spain's David Villa (L) scores his second goal during the FIFA World Cup 2010 group H preliminary round match between Spain and Honduras at the Ellis Park stadium in Johannesburg, South Africa, 21 June 2010. EPA/GEORGI LICOVSKI Please refer to www.epa.eu/downloads/FIFA-WorldCup2010-Terms-and-Conditions.pdf +++(c) dpa - Bildfunk+++
David Villa wa Uhispania akiipachika Honduras, bao la pili katika mchuano wa 21 Juni 2010, mjini Johannesburg, Afrika Kusini.Picha: AP

Sasa, Uhispania inapaswa kuifunga Chile, zitakapokumbana siku ya Ijumaa mjini Pretoria ili iweze kujipatia tikti ya kuingia katika duru ya pili ya michuano ya Kombe la Dunia.

Timu zilizofanikiwa kusonga mbele katika duru ya pili ni Uholanzi na Brazil. Cameroon na Korea ya Kaskazini zimeshatimuliwa katika duru hii ya kwanza.