1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kupanda kwa kiwango cha Joto - Mabadiliko ya hali ya hewa

26 Februari 2010

Viwango vya joto vinazidi kuongezeka barani Afrika, na hivyo kusababisha hali ya ukame, mafuriko na uhaba wa chakula. Sikiliza kwa makini ufahamu jukumu na mchango wako katika kubadilisha hali hii!

https://p.dw.com/p/MBbu
Mabadiliko ya hali ya hewa yanasababisha kiwango cha joto kuongezekaPicha: picture-alliance/dpa

Ingawa si kosa lako, hali hii inaendelea kutuathiri kwa kiwango kikubwa. Bara la Afrika ndilo litakalo athirika zaidi  na  mabadiliko ya hali ya hewa, licha ya kwamba bara la Ulaya na Marekani ndiyo yanayochangia pakubwa ongezeko la kiwango cha gesi ya Kaboni na moshi angani – chanzo kikubwa cha ongezeko la kiwango cha joto duniani. 

Ni bara la Afrika ambalo limo hatarini zaidi kwa sababu, bara hili hutegemea sana kilimo. Sehemu nyingi za bara hili zinakumbwa na ukame, mawimbi ya joto kali na misimu  isiyoweza kutabirika, hivyo kuifanya vigumu kuendesha shughuli za kilimo cha aina yoyote.

Je ni vipi  unaweza kushirikiana na wengine ulimenguni katika kampeni ya kupambana na  mabadiliko ya hali ya hewa kijijini mwako. Hilo ndilo swali wanalojiuliza Joshua, Carol, Lorna na Alex katika mchezo wa redio Noa Bongo jenga maisha yako kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa. Ni vijana wannne walioamua  kuchukua hatua ya  kupinga mradi wa ujenzi wa kiwanda  cha umeme kijijini mwao, na mwishowe  kujifunza mengi tu ya kushangaza kuhusiana na suala zima la mabadiliko ya hali ya hewa. 

Vipindi vya “Learning by Ear” ‘Noa bongo Jenga Maisha yako; vinasikika katika  lugha sita: Kiingereza, Kifaransa, Kiswahili, Hausa, Kireno na Amharic. Na vinafadhiliwa na wizara ya mambo ya nchi za kigeni ya Ujerumani.