1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kura ya maoni Misri; Desemba 15

2 Desemba 2012

Rais Mursi wa Misri ameitisha kura ya maoni Desemba 15 kuhusiana na katiba mpya, kwa matumaini ya kumaliza maandamano baada ya tamko lake la kujilimbikizia madaraka,wakati waungaji wake mkono wakiandamana mjini Cairo.

https://p.dw.com/p/16uKF
FILE - In this Friday, July 13, 2012 file photo, Egyptian President Mohammed Morsi speaks to reporters during a joint news conference with Tunisian President Moncef Marzouki, unseen, at the Presidential palace in Cairo, Egypt. Egypt’s Islamist president may hail from the fiercely anti-Israeli Muslim Brotherhood, but in his first major crisis over Israel, he is behaving much like his predecessor, Hosni Mubarak:. He recalled the ambassador and engaged in empty rhetoric supporting Palestinians. Mohammed Morsi is under pressure at home to do more but he is just as wary as Mubarak about straining ties with the United States. (Foto:Maya Alleruzzo, File/AP/dapd)
Rais wa Misri Mohammed MursiPicha: AP

Uidhinishaji wa katiba hiyo iliyotayarishwa na baraza ambalo linadhibitiwa kwa kiasi kikubwa na washirika wake wa makundi ya Kiislamu, utaondoa amri iliyotolewa Novemba 22 ambayo kwa muda inamkinga Mursi dhidi ya uchunguzi wa mahakama na kuzusha matamshi ya kuonyesha wasi wasi kutoka kwa mataifa ya magharibi.

Amri hiyo iliitumbukiza nchi hiyo katika mzozo wake mbaya kabisa kuwahi kutokea tangu pale Mursi aliposhinda katika uchaguzi mwezi Juni na kuzusha maandamano nchi nzima pamoja na ghasia ambamo watu wawili walipoteza maisha na mamia wamejeruhiwa.

In this image made with a mobile phone camera, supporters of Egyptian President Mohammed Morsi march in Cairo, Egypt, Saturday, Dec. 1, 2012. Thousands of people waving Egyptian flags and hoisting large pictures of the president demonsteated across Egypt in support of the president. The Muslim Brotherhood, from which President Morsi hails, hopes for a large turnout at the Saturday rallies to counter opposition protests. Hundreds of thousands of people took to the streets twice this week opposing Morsi’s decrees last week to grant himself sweeping powers. (Foto:Thomas Hartwell/AP/dapd)
Waungaji mkono rais Mursi wakiandamana mjini CairoPicha: AP

Uchumi waathirika

Hali hiyo imeathiri uchumi ambao ulikuwa unaonesha dalili za kufufuka.

"Narudia wito wangu wa kuanzisha majadaliano muhimu ya kitaifa kuhusiana na wasi wasi uliopo katika taifa , kwa moyo mkunjufu kabisa na bila kuelemea upande wowote," amesema Mursi baada ya kupokea mswada wa mwisho kutoka katika baraza la kutunga katiba. " Tunapaswa kusonga mbele na kuacha nyuma kipindi cha mivutano na kutofautiana, na kuanza kazi ya ujunzi wa taifa."

Katiba ina lengo la kuwa sehemu muhimu ya kuelekea katika demokrasia ya kweli baada ya miongo mitatu ya utawala wa kiimla uliokuwa ukiungwa mkono na jeshi chini ya uongozi wa rais Hosni Mubarak.

Hata hivyo utungaji wa katiba hiyo umeleta mgawanyiko, na kuweka wazi mipasuko kati ya makundi ya Kiislamu ambayo hivi sasa yanashikilia madaraka na wapinzani wao.

Source News Feed: EMEA Picture Service ,Germany Picture Service Protesters against President Mohamed Mursi are seen gathered in Tahrir Square in Cairo in this general view taken November 30, 2012. An Islamist-led assembly raced through approval of a new constitution for Egypt on Friday to end a crisis over Mursi's newly expanded powers, but opponents responded with another rally in Cairo against the Islamist leader. REUTERS/Mohamed Abd El Ghany (EGYPT - Tags: POLITICS CIVIL UNREST)
Waandamanaji wakiwa katika uwanja wa TahrirPicha: Reuters

Katiba ina mapungufu

Maandamano katika uwanja wa Tahrir mjini Cairo, eneo ambalo limekuwa kitovu cha maandamano dhidi ya Mubarak, wamekishutumu chama cha Mursi cha udugu wa Kiislamu katika kujaribu kulazimisha kuwa na katiba ambayo inamapungufu.

epa03199251 Nobel Peace Prize winner and former head of the International Atomic Energy Agency, Mohamed ElBaradei (C) is surrounded by his supporters and media as he arrives to announce the launch of the new 'Adoustour' (the Constitution in Arabic) Party in a press conference at the Egyptian Press Syndicate in Cairo, Egypt, 28 April 2012. ElBaradei and a group of pro-revolution personalities announced officially on 28 April the launch of the new 'Adoustour' political party aiming at gathering the Egyptian revolutionaries. EPA/AMEL PAIN pixel
Mohammed El-BaradeiPicha: picture-alliance/dpa

Viongozi wakuu wa upinzani kama Mohammed El Baradei amesema katika tovuti ya kijamii ya twita kuwa " Mapambano yataendelea " licha ya kura ya maoni na kwamba mswada wa katiba " unakandamiza haki za msingi za uhuru."

Viongozi wenye msimamo wa wastani ambao ni pamoja na katibu mkuu wa zamani wa jumuiya ya mataifa ya Kiarabu , Arab League, Amr Moussa, wamejitoa kutoka katika baraza hilo la kutunga katiba mwezi uliopita, kama walivyofanya wawakilishi wa Wakristo wachache nchini Misri.

FILE - In this Sunday, April 22, 2012 file photo, Egyptian presidential candidate Amr Moussa gestures during a press conference at his residence in Cairo, Egypt. A panel of fundamentalist Islamic clerics has endorsed the candidate of the Muslim Brotherhood for president of Egypt, an attempt to prevent a split of the conservative Muslim voters. Despite the official unity, the presence of two strong Islamist candidates raised the possibility that the religious vote could be split, creating fierce competition with secular figures. One is former Arab League chief Amr Moussa, who is popular among many who fear a dominant Islamist influence.(Foto:Nasser Nasser, File/AP/dapd)
Katibu mkuu wa zamani wa Arab League Amr MoussaPicha: AP

Mswada huo wa katiba una lugha yenye mapungufu ya makundi ya Kiislamu ambayo wapinzani wanasema inaweza kutumiwa kudhoofisha ukosoaji dhidi ya kuendewa kinyume haki za binadamu.

Mwandishi: Sekione Kitojo / rtre
Mhariri: Iddi Ssessanga