1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Labadia aachia ngazi VFB Stuttgart

26 Agosti 2013

Bundesliga yapamba moto , baada ya michezo mitatu, kocha Bruno Labadia wa FVB Stuttgart kibarua chaota majani, Hali pia si nzuri kwa makocha Torsten Fink wa Humburg SV na Jens Keller wa Schalke 04.

https://p.dw.com/p/19WHi
ARCHIV - Fußball DFB-Pokal 1. Runde: BFC Dynamo Berlin - VfB Stuttgart am 04.08.2013 im Friedrich-Ludwig-Jahn Stadion in Berlin. Der Stuttgarter Trainer Bruno Labbadia kommt zum Spiel. Bruno Labbadia, der Trainer des Fußball-Bundesligisten VfB Stuttgart, ist mit seinem Image unzufrieden. «Es ärgert mich natürlich, dass ich als Mahner und als Bremser dargestellt werde. Das sehe ich anders», sagte der 47-Jährige den «Stuttgarter Nachrichten» (Dienstag-Ausgabe) in einem Interview. Foto: Hannibal/dpa (zu dpa 0800 vom 07.08.2013) +++(c) dpa - Bildfunk+++
Kocha wa zamani wa VFB Bruno LabbadiaPicha: picture-alliance/dpa

Hewa kwa kocha wa VFB Stuttgart ilizidi kuwa nyepesi na kuumiza kichwa kama mtu anayepanda mlima mrefu baada ya timu hiyo kigogo cha soka nchini Ujerumani kupokea kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya FC Augsburg jana Jumapili.

Mashabiki waliimba , Bruno aondolewe, tangu pale timu hiyo ilipopokea kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Bayer Leverkusen na jana kukubali kipigo cha bao 2-1 dhidi ya Augsburg. Kocha wa FC Augsburg Markus Weinzierl wakati huo huo amesema amefurahishwa na ushindi huo.

"Kwa hakika tumefurahi sana, hilo ni wazi. Nawapongeza pia wachezaji wangu kwa kupata ushindi katika mchezo huu. Ni faraja kubwa kabisa kwetu. Nafikiri, tulistahili pia kushinda, kwasababu katika kipindi cha kwanza tulikuwa tuko mbele kwa mabao 2-0, na tulikuwa tunafanya vizuri, na katika wakati sahihi tumeweza kupata mabao. Tulistahi pia kuongoza katika mchezo huo".

Fußball Bundesliga 3. Spieltag: FC Augsburg - VfB Stuttgart am 25.08.2013 in der SGL-Arena in Augsburg (Bayern). Augsburgs Halil Altintop (r) und Stuttgarts Christian Gentner kämpfen um den Ball. Foto: Stefan Puchner/dpa (Wichtiger Hinweis: Aufgrund der Akkreditierungsbestimmungen der DFL ist die Publikation und Weiterverwertung im Internet und in Online-Medien während des Spiels auf insgesamt fünfzehn Bilder pro Spiel begrenzt.) +++(c) dpa - Bildfunk+++
Pambano kati ya FC Augsburg -na VfB StuttgartPicha: picture-alliance/dpa

VFB Stuttgart ilisema inatosha na ahsante sana kwa kocha Bruno Labadia na kuachana na huduma zake kuanzia leo Jumatatu(26.08.2013).

Labadia ambaye alijiunga na Stuttgart mwishoni mwa mwaka 2010 , anakuwa kocha wa kwanza msimu huu kufutwa kazi baada ya michezo mitatu ya ligi.

STUTTGART, GERMANY - AUGUST 26: Thomas Schneider, new head coach of VfB Stuttgart attends the VfB Stuttgart press conference at Mercedes-Benz Arena on August 26, 2013 in Stuttgart, Germany. (Photo by Thomas Niedermueller/Bongarts/Getty Images)
Kocha mpya wa Stuttgart Thomas SchneiderPicha: Bongarts/Getty Images

Mshambuliaji huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 47, ambaye pia aliwahi kuifunza Bayer Leverkusen na Hamburg SV, aliiokoa Stuttgart dhidi ya kushuka daraja mwaka 2011 na kuiongoza hadi kuingia katika ligi ya Ulaya msimu uliofuata.

Alipata mafanikio makubwa katika klabu hiyo baada ya kufikia fainali ya kombe la shirikisho DFB Pokal msimu uliopita, ambapo ilishindwa tu kuhimili vishindo vya Bayern Munich ambayo ilikamilisha ushindi wa vikombe vitatu katika msimu mmoja.

Borussia yapeta

Mwanzoni mwa mchezo wa tatu wa Bundesliga Borussia Dortmund iliendeleza ushindi wake msimu huu dhidi ya Werder Bremen kwa bao 1-0 nyumbani , wakati Bayern Munich ilifanikiwa kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Nürnberg.

Bayer Leverkusen haikuachwa nyuma katika kundi hilo la timu tatu zilizoanza vizuri msimu huu, baada ya kupata tena ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Borussia Moenchengladbach. Dortmund inaongoza msimamo wa ligi ikifuatiwa na Bayer Leverkusen na Bayern Munich.

JERUSALEM, ISRAEL - JUNE 18: Thiago Alcantara of Spain poses with the trophy after winning the UEFA European U21 Championship final match against Italy at Teddy Stadium on June 18, 2013 in Jerusalem, Israel. (Photo by Alex Grimm/Getty Images)
Tthiago Alcantara wa Bayern MunichPicha: Getty Images

Wakati huo huo mabingwa wa Ulaya Bayern Munich watakuwa wageni wa Freiburg kesho Jumanne , wakiwania kunyakua ushindi wao wa nne mfululizo katika Bundesliga kabla ya kusafiri hadi mjini Prague ambapo itapambana na Chelsea katika taji la Ulaya la Super Cup.

Hata hivyo Bayern ilipata pigo mwishoni mwa juma baada ya kupata taarifa kuwa mchezaji wake mpya Thiago Alcantara anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa wiki saba kutokana na majeraha aliyoyapata katika mchezo dhidi ya Nürnberg na anatarajiwa kufanyiwa operesheni leo Jumatatu.

Manchester City kurudi sokoni

Mabao mawili kutoka kwa Fraizer Campbell yaliwapa ushindi wa kushangaza wa mabao 3-2 Cardiff City dhidi ya Manchester City jana Jumapili wakati timu hiyo inayoshiriki kwa mara ya kwanza katika Premier League ikisherehekea ushindi wake wa kukumbukwa katika ligi hiyo nyumbani katika muda wa miaka 51.

Manchester City huenda wakaingia sokoni tena kusaka wachezaji wa ulinzi baada ya kipigo hicho cha kushitua, kilichoweka wazi matatizo ya ulinzi.

Katika michezo mingine jana Tottenham Hot Spurs ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Swansea City. Wakati siku ya Jumamosi Lukas Podolski ambaye kuwa uvumi kuwa huenda akarejea katika Bundesliga katika timu ya Schalke 04 kabla ya mwishoni mwa mwezi huu , alipachika mabao mawili katika ushindi wa timu yake ya Arsenal London wa mabao 3-1 dhidi ya Fulham.

Manchester United inamiadi leo usiku na Chelsea katika mchezo ambao unazikutanisha timu mbili ambazo zinaonekana zitakabana koo katika kuwania ubingwa wa Premier League msimu huu.

Real Madrid's coach Jose Mourinho (L) reacts beside Borussia Dortmund's coach Juergen Klopp during their Champions League semi-final first leg soccer match in Dortmund April 24, 2013. REUTERS/Wolfgang Rattay (GERMANY - Tags: SPORT SOCCER)
Kocha wa Chelsea Jose MourinhoPicha: Reuters

Wakati huo huo vita ya maneno imeanza kati ya Chelsea na Manchester United, sio kuhusu mchezo wao huo jioni ya leo lakini ni kuhusu mshambuliaji Wayne Rooney.

Kocha wa Chelsea Jose Mourinho amesema kuwa kocha wa Manchester United David Moyes anapaswa kubeba lawama kutokana na nia ya Wayne Rooney kutaka kuihama timu hiyo ya Old Trafford. Chelsea imetoa ombi la kumtaka Rooney kujiunga na timu hiyo mara mbili na haijaondoa uwezekano wa kufanya hivyo tena.

Rooney anasemekana kuwa amekasirishwa na matamshi ya Moyes kuwa atakuwa chaguo la pili iwapo Robin van Persie atakuwa majeruhi. Alipoulizwa Mourinho iwapo anatarajia hasira za mashabiki wa Manchester jioni ya leo alijibu, na hapa namnukuu ; hawastahili kupambana na mimi, iwapo nitasema Ramires atakuwa chaguo la pili wakati Frank Lampard atakuwa amechoka ama majeruhi, na iwapo mtu atakuja hapa na kumhitaji Ramires hakuna mtu atakayekasirika. Mwisho wa kumnukuu.

Barca yanusurika

FC Barcelona iliweza kunusurika mara kadha katika kipindi cha pili dhidi ya mashambulio ya Malaga na kufanikiwa kuibuka na ushindi mwembamba wa bao 1-0 jana Jumapili na kuendeleza mwanzo mzuri katika msimu huu. Wakati huo huo Atletico Madrid ambayo iko nafasi ya pili katika msimamo wa ligi ya Uhispania La Liga ilipata karamu ya magoli dhidi ya Rayo Valecano kwa kuigaragaza kwa mabao 5-0 jana Jumapili.

Nchini Italia Carlos Tevez alipata bao lake la kwanza katika ligi ya nchi hiyo Serie A baada ya mabingwa watetezi Juventus Turin ilipopata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Sampdoria . Napoli iliishinda Bologna kwa mabao 3-0.

Nchini Ufaransa Paris St Germain iliishinda Nantes kwa mabao 2-1 jana Jumapili, wakati Olympique Marseille ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Valenciennes siku ya Jumamosi.

Tanzia

Mlinda mlango Gilmar wa timu ya taifa ya Brazil ambayo ilipata ubingwa wa dunia mwaka 1958 na 1962 amefariki dunia mjini Sao Paolo akiwa na umri wa miaka 83. Mlinda mlango huyo wa zamani wa Santos FC na Corinthians amepata mshtuko wa moyo wiki iliyopita na hakuweza kuhimili hali hiyo hadi kufariki. Amekuwa katika hali mbaya ya afya kwa miaka kadha baada ya kupata kiharusi.

Kocha wa Tottenham Hotspurs Andre Villas-Boas amesisitiza kuwa uhamisho wa Gareth Bale kutoka timu hiyo kwenda Real Madrid haujakamilika, lakini anatarajia majadiliano yataendelea katika saa 48 zijazo.

Tottenham Hotspur's Gareth Bale celebrates after scoring the game-winning goal against West Ham United during their English Premier League soccer match in east London Tottenham Hotspur's Gareth Bale celebrates after scoring the game-winning goal against West Ham United during their English Premier League soccer match at Upton Park stadium in east London February 25, 2013. REUTERS/Eddie Keogh (BRITAIN - Tags: SPORT SOCCER) FOR EDITORIAL USE ONLY. NOT FOR SALE FOR MARKETING OR ADVERTISING CAMPAIGNS. EDITORIAL USE ONLY. NO USE WITH UNAUTHORIZED AUDIO, VIDEO, DATA, FIXTURE LISTS, CLUB/LEAGUE LOGOS OR 'LIVE' SERVICES. ONLINE IN-MATCH USE LIMITED TO 45 IMAGES, NO VIDEO EMULATION. NO USE IN BETTING, GAMES OR SINGLE CLUB/LEAGUE/PLAYER PUBLICATIONS.
Gareth BalePicha: Reuters

Bale alikuwa mjini Madrid wakati timu yake ilipopata ushindi dhidi ya Swasea City na kupata ushindi wa pili mfululizo katika Premier League.

Mbio za magari:

Sebastian Vettel amepata tena ushindi na dereva huyo wa Red Bull sasa ana points 46 mbele ya Fernando Alonso wa magari ya Ferrari katika msimamo wa Formula one kabla ya mbio zitakazofanyika huko barani Asia ambako Mjerumani huyo ametamba katika miaka iliyopita.

epa03738123 German Formula One driver Sebastian Vettel of Red Bull Racing kisses his trophy on the podium after winning the 2013 Canada Formula One Grand Prix at Gille Villeneuve circuit in Montreal, Canada, 09 June 2013. EPA/CJ GUNTHER +++(c) dpa - Bildfunk+++
Sebastian Vettel dereva wa Red Bull katika formula onePicha: picture-alliance/dpa

Katika mbio 14 zilizofanyika katika bara la Asia katika misimu mitatu iliyopita, Vettel ameshinda mara tisa.

Golf.

Wachezaji mahiri kutoka bara la ulaya na Asia watakabiliana kila baada ya miaka miwili katika kinyang'anyiro kipya cha mchezo wa golf nchini Malaysia katika mtindo wa kombe la Ryder unaokutanisha wachezaji wa golf wa Ulaya na Marekani.

Mwandishi: Sekione Kitojo / afpe / ape / dpae / rtre

Mhariri: Yusuf Saumu