1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Libya yaomba boti, helikopta kukabili wahamiaji haramu

Sekione Kitojo
26 Aprili 2017

Libya inautaka Umoja wa Ulaya kuipatia maboti na helikopta kusaidia doria katika Bahari ya Mediterania kugundua meli zinazowasafirisha wahamiaji haramu wanaoelekea barani Ulaya kusaka maisha.

https://p.dw.com/p/2bx2N
Mittelmeer Küste Libyen Rettungsaktion Flüchtlinge
Picha: Reuters/D. Zammit Lupi

Serikali  ya  Ujerumani  inasema  orodha  ya  maombi  hayo  kwa  ajili  ya  kikosi  cha  Libya  cha  ulinzi  wa  pwani  pia inajumuisha , magari  ya  kubebea  wagonjwa, vifaa  vya  mawasiliano  na  vile  vinavyoweza  kutumika kuona  nyakati za  usiku. 

Kwa  mujibu  wa  jibu  la  serikali  ya  Ujerumani  kupitia  swali  lililoulizwa  bungeni  kutoka  kwa  mbunge  wa  chama  cha  Die Linke, halmashauri  ya  Umoja  wa  Ulaya  inatafakari  kuhusu ombi  hilo. 

Kituo cha  televisheni  ya  taifa  cha  ARD  nchini  Ujerumani  kimeripoti leo  kwamba  Libya  inataka  baadhi  ya  maboti  hayo  yawe na  silaha. 

Umoja  wa  Ulaya  unataka kuzuwia wahamiaji  kuvuka  bahari  na  kuingia  katika  bara  la  Ulaya  kutoka  nchi  hiyo  ya  Afrika Kaskazini, ambayo  imetumbukia  katika  machafuko tangu  mwaka  2011 baada  ya  kuangushwa  kutoka  madarakani  kiongozi  wa muda  mrefu, Moammar Gaddafi.