1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

LUBUMBASH:Watu 13 wauwawa kwenye ajali ya ndege ya mizigoI

27 Agosti 2007
https://p.dw.com/p/CBVf

Watu 13 wameuwawa na wawili kujeruhiwa kufuatia ajali ya ndege ndogo ya mizigo huko kusini mashariki mwa jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo.Ajali hiyo ilitokea hapo jana katika eneo la Kongolo.

Kwa mujibu wa Jean Claude Kabange mkuu wa shirika la kitaifa la habari ndege hiyo ilikuwa na watu 15 wafanyikazi watatu wa ndege hiyo wakiwa raia wa Urussi na wakongomani 13.Ni watu wawili tu walionusurika.

Ndege hiyo ya Urussi aina ya Antonov ilikuwa ikitokea Goma kilomita 500 kuelekea kaskazini mashariki.

Walionusurika ni pamoja na mtoto wa miaka miwili na kijana mmoja na wako hospitali.

Maafisa wanasema huenda ndege hiyo ilikuwa ikijaribu kugeuza kurudi ilikotoka baada ya rubani kuhisi inamatatizo ya kimitambo.