1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maandamano nchini Ufaransa kuendelea

Sekione Kitojo22 Oktoba 2010

Vyama sita vikuu vya wafanyakazi nchini Ufaransa vimetoa wito wa maandamano zaidi kupinga mpango wa pensheni wa serikali.

https://p.dw.com/p/PkbI
Wanawake wakishikilia bango katika maandamano.Picha: AP

Paris.

Vyama  sita  vikuu   vya  wafanyakazi  nchini  Ufaransa vimetoa  wito  kwa  wapinzani  wa  mageuzi  ya  mpango wa  pensheni   kufanya  maandamano  makubwa   kwa muda  wa  siku  mbili  zaidi  katika  wiki  zinazokuja  licha ya  kura  ya  mwisho  kutarajiwa  kupigwa  na  baraza  la Seneti   leo  Ijumaa. Rais  Nicolas  Sarkozy , ambaye anataka  kiwango  cha  chini  cha  umri  wa  kustaafu kiongezwe  kutoka   miaka  60  hadi  62  ili  kupunguza gharama , amevishutumu  vyama  vya  wafanyakazi   kwa kuvuruga  hatua  za   kufufua  uchumi   dhaifu  wa ufaransa. Jana  Alhamis  polisi  wa  kuzuwia  ghasia walipambana  na   vijana  mjini  Lyon  na  Poitiers  wakati wafanyakazi  waliogoma  wakiendelea   kuweka  vizuwizi katika   viwanda  12  vya  kusafishia  mafuta  na  robo  ya vituo  vya  kuuzia  mafuta  nchini  humo   havina  mafuta. Ni nusu  tu  ya   treni  ziendazo  mikoani  zimekuwa zikifanyakazi. Vyama  vya  wafanyakazi , ikiwa  ni  pamoja na  chama  chenye  nguvu  cha  CGT, vimepanga maandamano   Alhamis  ijayo  na  Novemba  6.  Hatua  za kushughulikia  maandano  hayo  zinazochukuliwa  na  rais Sarkozy  zinaangaliwa  kwa  karibu  na  serikali  nyingine za  umoja  wa  Ulaya   ambazo  nazo  zinapanga  hatua  za kubana  matumizi.

Mwandishi : Sekione Kitojo / RTRE