Magazetini: Hukumu dhidi ya kundi la Freital ,hapa Ujerumani
8 Machi 2018Gazeti la Badische Zeitung la mjini Freiburg kuhusiana na hukumu iliyotolewa dhidi ya kundi linalojulikana kama Freital la msimamo mikali ya mrengo wa kulia, gazeti linaandika.
Kutokana na hukumu dhidi ya wanachama wa kundi ambalo sio tu walikuwa wakijaribu kuuwa, na hata kujenga kundi la kigaidi, hatua zimechukuliwa na msingi wa kuzima hali hiyo umewekwa. Hata wale ambao wameacha ugaidi ni magaidi. Mashitaka yaliwahusu kundi lililojificha katika ulinzi eti wa umma na baadaye kuzungumza katika mitandao ya kijamii kama makundi kwa siri wakitaka kufanya mashambulizi ya miripuko, hawawezi kusingizia, kwamba walikuwa tu ni baadhi ya watu waliokubaliana kufanya hivyo na sio wote waliotaka kuwauwa watu waliokuwa wakiomba hifadhi. Ndio, ni kweli : kumekuwa hivi karibuni katika maeneo ya Ujerumani mashariki na maandamano makubwa. Ambapo waungwaji wake mkono walikuwa wakitoa kauli mbiu iliyokuwa inakera , lakini kutokana na uhuru wa kutoa maoni haikuweza kuzimwa. Hawakuonekana kuwa wanakwenda kinyume na ubinadamu.
Kila mmoja katika Freital alifahamu kuhusiana na uhalifu wa kundi la wanazi mamboleo, ni polisi tu hawakuwa na habari. Anaandika mhariri wa gazeti la Märkische Oderzeitung la mjini Frankfurt / Oder akizungumzia kuhusu hukumu hiyo iliyotolewa dhidi ya kundi la kigaidi ya wanazi mamboleo mjini Freital. Mhariri anaandika.
Kuna maafisa wengi wanaowaunga mkono magaidi. Takriban polisi mmoja aliwahi kuwa mtu anayetoa taarifa kwa kundi hilo la misimamo mikali ya mrengo wa kulia. Na mahakama ya Saxon haikuona hamasa za kisiasa kwa wahalifu hao. Licha ya mwelekeo wa kupinga wakimbizi na makundi ya mrengo wa kushoto. Lengo gani basi lilitakiwa kuonekana hapa? Anauliza mhariri.
Vita vya kibiashara
Kuhusiana na vita vya kibiashara kati ya Umoja wa Ulaya na Marekani , mhariri wa gazeti la Neue Osnabrücker anaandika:
Halmashauri ya Umoja wa Ulaya imechukua hatua, lakini sio kwa hatua ilizochukua Marekani kwa kutangaza kupandisha kodi kwa biadhaa kama chuma cha pua na aluminium. Ni sawa kwani cheche huzaa moto. Hiki ni kitisho cha vita ya kibiashara, ambayo ni mshindwa tu anafahamu. Kuonesha ishara ni muhimu. Ni kwa njia hiyo tu huenda rais wa Marekani Donald Trump , anaweza kutambua, ni wapi kujihami kimasoko kunaweza kumpeleka. Lakini iwapo Umoja wa ulaya inaongeza kodi kwa biadhaa kama siagi ya karanga, vinjwaji vikali kama wiski, nguo za Jeans na pikipiki, kwa mtazamo wa haraka inaonekana kama ni hatua dhaifu. Hizi hata hivyo ni bidhaa maarufu sana za Marekani. Na hatua hizi zinaleta hali ya tahadhari.
Iwapo inawezekana kumzuwia rais Trump kwa kupandisha kodi za bidhaa kama juisi ya machungwa kutoka Califonia ama Cranberi, itabidi kusubiri na kuona. Anaandika mhariri wa gazeti la Rhein-Zeitung la mjini Koblenz kuhusiana na kitisho cha vita ya kibiashara kati ya Marekani na Umoja wa Ulaya. Mhariri anaandika.
Hatari inaonekana zaidi katika kuweka ongezeko la kodi katika kila bidhaa. Kwa hatua kama hizo hakuna atakayeshinda. Trump hawezi kupata faida kwa upande wa biashara ya chuma cha pua na Umoja wa Ulaya hautaweza kufikia katika lengo la soko huru.
Ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu hauvifikii vyombo vingi vya habari. Anaandika mhariri wa gazeti la Weser-Kurier la mjini Bremen kuhusiana na ripoti ya haki za binadamu ya Umoja wa mataifa. Mhariri anaandika:
Hakua taarifa zilizojitokeza za uhuru wa kutoa habari nchini Cambodia muda mfupi kabla ya uchaguzi. Hakuna mtu aliyejua, kwamba wanawake nchini El Salvador wanahukumiwa kifungo cha muda mrefu, inapotokea ujauzito umetoka. Masuala ya kisiasa pia yanaundumila kuwili. Umoja wa Ulaya umeweka vikwazo vya kisiasa kwa utawala wa Venezuela, lakini watu wengi hawawezi kutoa kauli zao nchini Ukraine. Mhariri anasema suala la haki za binadamu limechukua mtazamo wa kimaslahi zaidi.
Mwandishi: Sekione Kitojo / inlandspresse
Mhariri: Mohammed Abdul Rahman