1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maoni ya wahariri.

Mtullya, Abdu Said6 Mei 2008

Katika maoni yao wahariri leo wanazungumzia juu ya tatizo la ulevi miongoni mwa vijana nchini Ujerumani.

https://p.dw.com/p/DuPw
Magazeti ya Ujerumani.Picha: DW / Görner

Wahariri wa  magazeti  kadhaa ,leo ,katika maoni yao  wanaliangalia  tatizo la ulevi miongoni mwa  vijana nchini Ujerumani. 

Gazeti la WESTFALEN POST linazungumzia  juu ya  mkasa wa maiti tatu za watoto wachanga zilizokutwa ndani ya friji.

Na mhariri  wa  gazeti la LEIPZIGER VOLKSZEITUNG  anapongeza  uamuzi juu ya kuwaadhibu vikali madereva wanaokimbia kana kwamba wanafukuzwa.

Ripoti mpya inaonesha kuwa  tatizo la ulevi linazidi kuwa kubwa miongoni  mwa vijana  nchini  Ujerumani. Gazeti la ALLGEMEINE ZEITUNG linauliza kwa nini vijana  wengi  wanatumia ulevi kama njia ya  kuyakabili maisha yao.

Mhariri wa gazeti hilo  anajibu swali lake kwa  kueleza  kuwa vijana  hao wanakunywa  pombe  sana kutokana na shinikizo la maisha kuzidi kuwa  kubwa katika jamii. Wanalazimika kuonesha uwezo  wa  ushindani  ambao hawana.

Gazeti  linafafanua kuwa vijana  hao hawana  mifano  bora  ya kuiga na ndiyo sababu kwamba mifumo  yao  ya maadili  imetenguka.Lakini mhariri wa gazeti hilo anawaambia  vijana wa kijerumani ;kuvuta na kulewa siyo suluhisho.

Mhariri wa gazeti  la DRESDENER NEUESTEN NACHRICHTEN  anaunga mkono wazo la kupiga  marufuku matangazo ya biashara juu ya sigara na ulevi .

Anasema anaeghabishwa na  tabia ya vijana wanaolewa ,kiasi cha kupoteza fahamu,hana budi aunge mkono hatua kali  za  kuzuia ulevi- ikiwa pamoja na kupiga  marufuku mambo yote yanayotukuza sigara na  pombe.

Mhariri  wa  gazeti la DRESDENER NEUESTEN  NACHRICHTEN anatilia maanani  kuwa  pombe sasa , imekuwa uraibu wa hatari miongoni  mwa vijana wa kijerumani.

Lakini,  mhariri huyo anasema  vijana hao  wanafuata mfano wa watu fulani, kwani  nchini  Ujerumani watu milioni kumi  wanautatika kupita kiasi.Vijana wanaiga  tu.

Mapema  wiki hii Ujerumani  ilishtushwa tena ,kutokana na habari juu ya  kukutwa maiti  tatu  za watoto wachanga  ndani ya friji. Juu ya hayo gazeti la WESTFALENPOST  linauliza vipi balaa kama hilo linaweza  kutokea  bila  mtu kujua.

Mhariri anauliza iwapo hakuna mtu alieomwona mama aliewabeba watoto hao tumboni. Jee hakuna mtu aliemwona  mama  huyo alivyokuwa mjamzito mara tatu? Ili kuepusha  balaa kama hilo mhariri anashauri juu ya kuweka vitengo vya msaada, ambapo akina  mama wanaweza kupeleka watoto  ikiwa wanashindwa kuwahudumia.