Rais John Magufuli wa Tanzania amewataka Watanzania kuanzia leo Ijumaa kutenga muda wa siku tatu hadi Jumapili kufanya maombi maamulu kwa ajili ya kudhibiti virusi vya Corona. Hii ni mara ya kwanza tangu janga hilo kupiga hodi katika nchi za Afrika kwa kiongozi wa nchi kutaka wananchi wake kutenga muda wa siku hizo kwa ajili ya kufanya maombi dhidi ya Corona. George Njogopa alituarifu.