1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maoni: Urithi wenye sumu wa Brexit anaoacha Theresa May

Sekione Kitojo
7 Juni 2019

Tarehe 7 Mei, ni siku ambayo waziri mkuu  wa Uingereza Theresa May alitangaza atajiuzulu wadhifa wake kutokana na shinikizo la viongozi wa chama chake cha Conservative kumtaka afanye hivyo, kutokana na mkwamo wa Brexit.

https://p.dw.com/p/3K0TK
Belgien, Brüssel: Theresa May
Picha: picture-alliance/AP/V. Mayo

Katika maoni yake mwandishi wa DW, Rob Mudge  anaandika  kwamba , msizubaishwe  na machozi aliyoyamwaga May wakati  akiaga. Waziri  mkuu  May alipitia katika  mchakato  wa  Brexit  ambao umekatikakatika  na  usiofanya kazi na  ameiacha  nchi hiyo katika  hali inayoshitua ya kama ugonjwa wa kupooza. 

Belgien, Brüssel: Theresa May
Theresa May, waziri mkuu wa UingerezaPicha: picture-alliance/dpa/A. Vitvitsky

Kwa  hiyo  basi  Theresa  May  anaelekea  binafsi  katika  chochote kile  ambacho  atajaliwa katika  maisha yake  ya  baada ya waziri mkuu. Hali ya  baadaye  ya  nchi  yake , ambayo anajigamba  kwamba  anaipenda, imo  katika  hali  ngumu  zaidi, kama sio katika  hali  ambayo inaweza  kusemwa  kwa  kebehi, "asante kwa msimamo wake  wa mkanganyiko, mtengano  na  uongo wa  Brexit."

Lakini  sio  tu imani yake ya kufikirika kwa  kuamini  kwamba  anaweza kufanikisha kile  alichosema  ni "bora kwa  nchi  yake." Ni vile alivyojaribu  kuuza  imani  hiyo  katika  Umoja  wa  Ulaya  mjini  Brussels na  katika  baraza  la  wawakilishi. Wanasema  kwamba muonekano unadanganya, lakini  alivyokuwa  akijitokeza  hadharani, ambako kumejitokeza  kuashiria kutokuwa  na  hisia na hali ya wasiwasi, na taswira inayoonesha  kila  mara kama  panya aliyekabiliwa  usiku  na taa za  gari, haikumuonesha  kuwa karibu  na  nchi  ambayo  imegawika na  kuongezeka mtengano.

Kuungama May

Na bila  shaka sina  imani  na  mtu ambaye  kuungama  kwake  kufanya kitu cha  utundu, eti  ni kuwa  alikuwa  akikimbia  katika  mashamba  ya ngano  wakati  akiwa  mtoto. Katika  anguko  moja  hakukamilisha  tu hatma yake  lakini  bila  shaka  ile  ya  vizazi vingine  vijavyo kwa  tamko lake  la  "kutopata makubaliano  ni  bora  kuliko makubaliano  mabaya." Kwa hiyo, inaonesha kutowajibika  kabisa. Katika  hali ambayo  ni mbaya, jaribio  lake  la  kutumia  mamlaka  yake  ya  waziri  mkuu kuhalalisha  dhana  yake  hiyo ya  uongo, haitasameheka.

Brexit - Labour leader Jeremy Corbyn
Kiongozi wa chama cha Labour Jeremy CorbynPicha: picture-alliance/A. Chown

Kama  Muingereza  anayefanya kazi  nchini  Ujerumani, sina bahati mbaya  ya  kuamka  kila  siku na  hisia  za  kudidimia katika  nchi ambayo inadidimia. Lakini  nilikuwa  mjini  London kwa  ajili  ya  kura  ya kwanza  ya  wananchi  Oktoba  mwaka  jana, na  kushuhudia  hasira, kukata  tamaa lakini  pia  dhamira  ya  mamia  kwa  maelfu ya  watu, vijana  na  wazee, ambao  walikuwa  wakipambana  kwa  amani  kujaribu na  kuzuwia  nchi  yao kupotea katika lile tundu, liitwalo tundu  jeusi.

May  na  bila  kusahau  kiongozi  wa  chama  cha  Labour Jeremy Corbyn, ambaye anafanana  na  May  katika kuyumbayumba kwao, wamechagua  kupuuzia matakwa  ya  wananchi. Mtazamo wao haukwenda  sambamba  na  ule  wa  wananchi  waliopiga kura  mwaka 2016  kujitoa  kutoka  Umoja  wa  Ulaya.