1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maoni: von der Leyen ndie rais mpya wa halmashauri ya Ulaya

Sekione Kitojo
17 Julai 2019

Ursula von der Leyen ameonesha katika bunge la Ulaya katika enzi hizi za Internet inawezekana kutamka neno na likaweza kubadilisha mambo. Ndivyo alivyofanya von der Leyen .

https://p.dw.com/p/3MBjh
Frankreich Wahl zur EU-Kommissionspräsidentin | Ursula von der Leyen | Rede nach Bestätigung
Picha: Reuters/V. Kessler

Mhariri  anaandika  kuwa  mara hii  ilikuwa  tofauti, ilikuwa siku  ambapo mgombea  huyo kutoka  Ujerumani kila  kitu kiliwezekana. Alilazimika kulidhibiti  jukwaa  la  bunge la  Ulaya. Akalazimika   kuwashawishi wale  waliokuwa  wakimtilia shaka, akaliimarisha kundi  la  wale waliokuwa  wakimuunga  mkono, na wapinzani  akawaweka  katika  njia ambamo wanaweza kumuunga  mkono. Na anatakiwa  kushughulikia masuala  ya  Ulaya.

Kila kundi lilimpigia  kura Ursula von der Leyen, hata  kama hatimaye  ulikuwa  ushindi mwembamba kwa  kura  tisa tu. Mwanamke  huyu mwenye msimamo wa utetezi  wa  wanawake  alijionesha kuwa  ni mtetezi  wa  masuala  ya kijamii  na  mlinzi  wa  mazingira kama  wengi wa wanachama  wenzake katika chama  chake, na alionesha  kujiamini  na kwamba ni  mwanamke  anayeweza.

Huenda  lilikuwa  wazo lake  bora hotuba yake  kuizungumza katika  lugha  tatu. Kifaransa kutokana  na  hisia za nguvu za uwakilishi  wa  umma, Kiingereza, kutokana  na  ukweli ulio mgumu pamoja  na  mahitaji, kutokana na kiwango  kikubwa  cha uendeshaji wa uchumi  mkubwa na kupata  haki  sawa  wa kijinsia.

04 | Interview Armin Laschet, Ines Pohl
Ines Pohl mhariri mkuu , Deutsche WellePicha: DW/R. Oberhammer

Wajerumani  walimchagua  baada ya  kufikia  uamuzi  kuwa mwanasiasa  huyo  aliyezaliwa mjini Brussels, majaaliwa  yake  ni kama  yameelekezwa  katika kufanyakazi  katika  Umoja huo.

Si  siri  tena, kwamba  von der Leyen  kwa  wadhifa  huu  alikuwa ni  chaguo  la  pili. Anafahamu , kwamba  anapaswa  kupambana  na hali  hii. Angeweza kupoteza kila  kitu. Lakini  ameleta mshangao  na  kutoka kuwa  chini amejiweka  juu. Amewaacha  hoi wale  ambao  hawapendelei Umoja wa  Ulaya  na  wale  wanaotaka kujitoa kutoka  Umoja  huo. Njia hii  ni  lazima  aiendeleze  na kulizuwia  kundi  la  mrengo  wa kulia.

Hayo  yote , hata  hivyo hayahakikishi kuwa na  urais  wa mafanikio  katika  halmashauri ya  Umoja  wa  Ulaya , lakini  ni mwanzo  mzuri  na  ni  siku  nzuri kwa  bunge  la  Ulaya, kwamba kulikuwa  na  uchaguzi  halisi.

Kundi  ambalo  limeshindwa  kwa kiasi  kikubwa  katika  siku  hii ya  uchaguzi ni wabunge  wa Ulaya  wa  Ujerumani  wa kutoka wa chama  cha  Social democratic. Walitaka  kwa  njia  zote  kuwe na  makubaliano  ya  mgombea wao  ashike  wadhifa  huo.