1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mapigano mapya yazuka Libya watu 40 wauawa

17 Novemba 2013

Mapigano mapya yamezuka mjini Tripoli Libya jana Jumamosi(16.11.2013) wakati idadi ya watu waliouawa katika mapigano wakati wa maandamano ya kupinga wanamgambo ikipanda na kufikia watu 43.

https://p.dw.com/p/1AIxn
Protesters march during a demonstration calling on militiamen to leave, in Tripoli November 15, 2013. At least 10 people were wounded in Tripoli on Friday when militiamen opened fire on hundreds of protesters who had marched on their brigade headquarters to demand that they leave the Libyan capital, a Reuters witness said. Heavy smoke could be seen from the scene as Libyan police and armed local residents battled to control the militiamen in an area on the road to Tripoli's international airport. REUTERS/Ismail Zitouny (LIBYA - Tags: POLITICS CIVIL UNREST)
Waandamanaji mjini TripoliPicha: Reuters

Zaidi ya watu 450 wamejeruhiwa wakati maandamano siku ya ijumaa yalipozusha mapigano katika mji huo mkuu baina ya makundi ya wanamgambo ambayo yaliendelea usiku kucha , amesema waziri wa sheria Salah al-Marghani.

Waziri mkuu Ali Zeidan, ambaye alitekwa nyara kwa muda na wanamgambo mwezi uliopita katika tukio ambalo linaelezea hali inayoongezeka ya kutokuwa na uthabiti , ametoa wito wa "kuvumiliana na kusitishwa kwa mapigano," akionya kuwa " muda unaokuja na siku zijazo zitakuwa muhimu katika historia ya nchi ya Libya".

Protesters march during a demonstration calling on militiamen to leave, in Tripoli November 15, 2013. At least 10 people were wounded in Tripoli on Friday when militiamen opened fire on hundreds of protesters who had marched on their brigade headquarters to demand that they leave the Libyan capital, a Reuters witness said. Heavy smoke could be seen from the scene as Libyan police and armed local residents battled to control the militiamen in an area on the road to Tripoli's international airport. REUTERS/Ismail Zitouny (LIBYA - Tags: POLITICS CIVIL UNREST)
Mandamano yakiendelea mjini TripoliPicha: Reuters

Maafisa watangaza mgomo

Usiku wa Jumamosi , maafisa wa mji wa Tripoli wametangaza , "mgomo wa nchi nzima wa siku tatu katika sekta ya umma na binafsi kuanzia Jumapili" ikiwa ni jibu kutokana na ghasia hizo. Nchi hiyo imeshuhudia ongezeko la hali isiyo tulivu wakati waasi wa zamani ambao walisaidia kuuangusha kutoka madarakani utawala wa Muammar Gaddafi uliodumu miongo kadha mwaka 2011, walipuuzia madai ya serikali ya kutaka waweke silaha zao chini.

Ghasia hizo mpya zilizuka wakati waandamanaji wakiwa wamebeba bendera nyeupe walioingia mitaani katika maeneo ya majengo ya kifahari ambayo yanatumika kama kituo cha kikosi cha Misrata, kinachoundwa na wapiganaji waliokomaa kwa vita kutoka mji wa magharibi wa Misrata, na wakidai kuwa wanamgambo hao waondoke mjini humo.

AUSSCHNITT ATTENTION EDITORS - VISUAL COVERAGE OF SCENES OF INJURY OR DEATH People carry a man who was injured when Libyan militiamen opened fire into a crowd of protesters in Tripoli November 15, 2013. Six people were killed and dozens more wounded in clashes between militiamen and armed residents in the capital Tripoli on Friday, state television said, in a further challenge to Libya's weak government. The bloodshed began when militiamen opened fire into hundreds of protesters demanding their eviction from the capital after they had repeatedly battled with other armed factions for control of parts of the capital. REUTERS/Stringer (LIBYA - Tags: POLITICS CIVIL UNREST) TEMPLATE OUT
Watu waliojeruhiwa baada ya kushambuliwa na wanamgamboPicha: Reuters

Watu wenye silaha walifyatua risasi kutoka ndani ya nyumba hizo katika eneo la Gharghour, na kuuwa waandamanaji kadha na kusababisha wanamgambo wa makundi mengine kushambulia kituo hicho cha wanamgambo wa Misrata, na kuchoma sehemu ya eneo hilo.

Mji wa pwani wa Misrata, ulioko kilomita 200 mashariki ya mji ya Tripoli, umeshuhudia mapigano makubwa kabisa kuwahi kutokea tangu vuguvugu la maandamano ya umma ya mwaka 2011.

Kikosi cha Misrata kilishambulia kambi ya jeshi mapema jana Jumamosi(16.11.2013) , na kuzusha duru nyingine ya mapambano ambapo mtu mmoja ameuwawa na wengine wanane wamejeruhiwa, kwa mujibu wa kanali Mosbah al-Harna, kamanda wa kikosi kingine ambacho kwa kawaida kiko chini ya mamlaka ya wizara ya ulinzi.

Harna amesema wanamgambo wa kikosi cha Misrata baadaye walipora kituo hicho cha jeshi, wakichukua magari, silaha na risasi.

Libya's Prime Minister Ali Zeidan places his hand on his forehead as he addresses a news conference after his release and arrival at the headquarters of the Prime Minister's Office in Tripoli October 10, 2013. Zeidan was seized and held for several hours on Thursday by former rebel militiamen angry at the weekend capture by U.S. special forces of a Libyan al Qaeda suspect in Tripoli. REUTERS/Ismail Zitouny (LIBYA - Tags: POLITICS CIVIL UNREST TPX IMAGES OF THE DAY)
Waziri mkuu wa Libya Ali ZeidanPicha: Reuters

Wapiganaji wengi zaidi kutoka Misrata walijaribu kuingia mjini Tripoli kutoka upande wa mashariki, na kuzusha mapigano na wanamgambo hasimu kabla ya mlolongo wa wanamgambo hao wa ziada kurejea nyuma kwa kilometa kadha.

Ngao ya Libya

Kikosi cha "Ngao ya Libya" ambacho ni kikosi kingine cha waasi wa zamani ambacho kilikuwa chini ya udhibiti wa serikali , baadaye kilitangaza kuwa kinalidhibiti eneo la Gharghour wakati wapiganaji wa Misrata wakijitoa katika eneo hilo.

Kikosi cha Ngao ya libya katika eneo lenye matatizo la mji wa mashariki wa Benghazi nacho kilikuwa lengo la maandamano mwezi Juni ambayo pia yalisababisha umwagikaji wa damu, ambapo watu zaidi ya 30 walipoteza maisha.

Members of the Libyan security forces stand guard close to the headquarters of the General National Congress in Tripoli October 31, 2012. Protesters stormed Libya's national assembly on Tuesday, forcing the cancellation of a vote on a proposed coalition government named by the country's new prime minister just hours earlier. REUTERS/Ismail Zitouny (LIBYA - Tags: POLITICS CIVIL UNREST)
Jeshi likilinda maeneo kuzuwia wapiganaji wa Misrata kuingia mjini TripoliPicha: Reuters

Barabara kuelekea mji wa Tripoli kutoka upande wa mashariki imefungwa , amesema mwandishi mmoja wa shirika la habari la AFP,na mji huo sasa uko shwari hadi jana jumamosi, lakini shughuli nyingi za kibiashara na maduka zimefungwa.

Mwandishi : Sekione Kitojo / afpe

Mhariri: Amina Abubakar