1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maroketi yashambulia makazi ya Rais Saleh

Mnette,Sudi/rtre,afpe4 Juni 2011

Rais Ali Abdullah Saleh wa Yemen ametoa wito kwa vikosi vyake kuchukua hatua dhidi ya kile alichokiita, "magenge yenye silaha" saa chache baada ya maroketi kushambulia makazi yake.

https://p.dw.com/p/RRks
Fire and smokes erupt during clashes between tribesmen loyal to Sheik Sadeq al-Ahmar, the head of the powerful Hashid tribe, and Yemeni security forces in Sanaa, Yemen, late Thursday, June 2, 2011. Thousands of tribesmen threatened Thursday to descend on Yemen's capital to join the battle against forces loyal to President Ali Abdullah Saleh as the country slid deeper into an all-out fight for power. Government forces in Sanaa unleashed some of the heaviest shelling yet against their tribal rivals in a dramatic escalation of the conflict. (AP Photo/Mohammed Hamoud)
Mapambano yashika kasi mji mkuu wa Yemen,SanaaPicha: dapd

Watu 7 wameuawa katika shambulio hilo mjini Sanaa. Waziri Mkuu na Spika wa Bunge ni miongoni mwa watu waliojeruhiwa. Rais Saleh, amesema kuwa yeye ni mzima na amelilaumu kundi la kikabila kwa mashambulizi hayo.Sheikh Sadiq al-Ahmar, anaeongoza muungano wa kikabila unaotaka kumuondoa Saleh madarakani, amekana kuhusika na shambulio hilo.

Nae Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya Catherine Ashton amesema, kuna mpango wa kuwahamisha raia wa umoja huo kutoka Yemen kwa sababu ya machafuko yanayozidi kushika kasi nchini humo.