1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mazungumzo nyeti kati ya Israel na Wapalestina kuanza leo

14 Januari 2008
https://p.dw.com/p/CpAW

JERUSALEM

Wasuluhishi waandamizi wa Israel na Palestina leo wanatazamiwa kuanza mazungumzo kama sehemu ya shinikizo la Marekani la kufikiwa kwa makubaliano ya amani kabla ya kumalizika kwa mwaka huu.

Rais Mahamoud Abbas wa Wapalestina amesema msuluhishi wake mkuu Ahmed Qorei na waziri wa mambo ya nje wa Israel Tzipi Livni wataongoza mazungumzo hayo juu ya masuala muhimu ambayo wanataraji yatapelekea kuundwa kwa taifa huru la Wapalestina.

Masuala hayo yanajumuisha mustakbali wa mji wa Jerusalem, uchoraji wa mipaka na hatima ya wakimbizi wa Kipalestina.