1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Medved amuomba Putin kuongoza serikali yake

11 Desemba 2007
https://p.dw.com/p/CaIS

MOSCOW.Dmitry Medvedev ambaye ametajwa na Rais Vladmir kumridhi kiti cha Urais amesema kuwa anataka rais huyo kuwa waziri mkuu katika serikali yake, hatua inayoashiria kuendelea kwa Putin kushika hatamu.

Hata hivyo Putin mwenyewe hajasema kama atakubaliana na nafasi hiyo ya mfuasi mkubwa wa muda mrefu.

Wadadisi wanasema kuwa kiongozi huyo mwenye nguvu bado hajaamua nafasi atakayoitumikia baada ya kung´atuka madarakani mwezi March mwakani.

Katika hotuba yake fupi kwa njia ya televisheni, Medvedev alisema.