1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MELBOURNE : Maandamano yapinga utandawazi

18 Novemba 2006
https://p.dw.com/p/CCrf
Wakimbizi wa Tchad
Wakimbizi wa TchadPicha: AP

Waandamanaji wanaopinga utandawazi wamepambana na polisi katika mji wa Melbourne nchini Australia kupinga mkutano wa mawaziri wa fedha na magavana wa benki kuu kutoka nchi za kundi la mataifa 20 yenye maendeleo ya viwanda duniani.

Maafisa waandamizi wa Benki ya Dunia na wa Shirika la Fedha la Kimataifa ni miongoni mwa wanaohudhuria mkutano huo.

Maandamano ya kuupinga mkutano huo yamefanyika licha ya kuwepo kwa msako mkubwa wa usalama katika mitaa ilioko karibu na eneo la mkutano ambalo limefungwa kwa vizuizi vya barabarani pamoja na kufungwa kwa njia.