1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Messi hatimaye acheka na wavu

7 Oktoba 2019

Barcelona waliwanyeshea Sevilla mabao mane kwa bila uwanjani Camp Nou katika La Liga, huku Lionel Messi akiutilia kikomo ukame wake mdogo wa magoli kwa kufunga bao katika mtanange huo.

https://p.dw.com/p/3QqSa
Spanien Fußball FC Barcelona - UD Levante Lionel Messi
Picha: picture-alliance/dpa/M. Fernandez

Kufunga kwa Messi ni habari njema kwa Messi kuelekea mtananga wa El Clasico utakaopigwa baada ya mechi ijayo ya La Liga.

Barca kwa sasa wanaishikilia nafasi ya pili nyuma ya Real Madrid halafu Atletico Madrid wako katika nafasi ya tatu baada ya kutoka sare ya kutofungana na Real Valladolid.