1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mgogoro kuhusu umilikaji wa visiwa baina ya China na Japan

18 Septemba 2012

Kwa siku sasa maelfu ya Wachina wamekuwa wakifanya maandamano katika miji mbalimbali ya nchi yao kupinga hatua za Japan kutaka kuvimiliki visiwa vidogo vya Senkaku vilioko katika bahari baina ya nchi hizo mbili.

https://p.dw.com/p/16B8V
Waandamanaji wa Kichina wachoma moto bendera ya Japan
Waandamanaji wa Kichina wachoma moto bendera ya JapanPicha: AP

Maandamano hayo, mingine ya hamasa kubwa na yakipita mbele ya ubalozi wa Japan mjini Beijing, yamezusha wasiwasi wa kimataifa na hofu baina ya nchi hizo mbili zenye uchumi mkubwa duniani. Kuna ripoti kwamba makampuni ya kijapani hivi sasa yanafungwa au kupunguza shughuli zao huko China.

Othman Miraji alizungumza na mwandishi wetu wa Beijing, Fadhili Mpunji, na akamuuliza uhasama huu unaangaliwa kwa kiasi gani huko China.

(Kusikiliza mazungumzo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini)

Mahojiano: Othman Miraji/ Fadhili Mpunji

Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman