1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mgomo wa reli wakaribia kumalizika Ufaransa

22 Novemba 2007
https://p.dw.com/p/CRtm

Mgomo wa reli uliokwamisha huduma za usafiri nchini Ufaransa tangu siku tisa zilizopita, unakaribia kumalizika.Madereva wengi wa treni walianza kurejea kazini baada ya majadiliano ya upatanisho kuanza mjini Paris.

Mgomo huo uliochochewa na mipango ya serikali kutaka kufanya mageuzi katika mfumo wa malipo ya uzeeni ya wafanyakazi wa mashirika ya reli, umesababisha hasara ya kama Euro milioni 400 kila siku moja.