1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Michezo:Bundesliga

9 Desemba 2007

---

https://p.dw.com/p/CZPi

MWISHOE:MICHEZO:

Bayern Munich wamebakia kileleni mwa Bundesliga-Ligi ya Ujerumani licha ya kwamba jana walimudu sare tu 0:0 na chipukizi Duisburg.katika mapambano mengine Bremen inayonyatia nafasi ya pili kileleni ililazwa na hannover 4-3 huku hamburg ikitoka nayo suluhu 0:0 na Cottbus.Mabingwa watetezi Stuttgart waliizaba Wolfsburg 3:1.

Katika ringi ya mabondia:

FLOYD Mayweather Jr, ametetea taji lake la wezani wa Welterweight la ubingwa wa dunia la shirika la WBC.Huko Las Vegas, alimdengua mapema alfajiri ya leo muingereza Ricky Hatton katika duru ya 10 kufuatia makonde ya mchanganyiko kutoka kulia na kushoto.Mara 2 Hatton aliporomoka chini.