1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nchi tajiri zakubaliana kupunguza hewa chafu na kuendelea kushirikiana n...

Mtullya, Abdu Said9 Julai 2008

Nchi tajiri duniani zakubaliana kupunguza kwa nusu hewa chafu hadi ifikapo mwaka 2050.

https://p.dw.com/p/EZ8W
Kansela Angela Merkel wa Ujerumani na mwenyeji wa mkutano waziri mkuu wa Japan Yasuo Fukuda.Picha: AP

Baada  ya  mkutano wao  wa  siku  tatu nchini Japan  viongozi  wa  nchi 8 tajiri wamekubaliana  juu ya kupunguza  hewa chafu, kuzisaidia nchi za Afrika, pamoja na kukabiliana  na mifumuko ya bei za chakula na nishati.

Vingozi  wa  nchi hizo wamekubaliana kwa jumla  juu ya  kupunguza  kwa nusu utoaji wa  hewa  chafu, Co2 hadi kufikia mwaka 2050.

Lakini viongozi hao hawakufafanua  juu ya makubaliano yao ambayo hayakuungwa mkono na nchi zinazoinukia kiuchumi ,India na China.

Hatahivyo mkutano wa viongozi wa nchi za G8  umetathminiwa  kuwa wa mafanikio  na  Kansela  wa Ujerumani Angela Merkel hasa katika  suala la kupambana  na mabadiliko ya hali ya hewa.

Kansela Merkel pia amesema viongozi wa nchi tajiri wamekubaliana  juu ya kuimarisha  ushrikiano na nchi zinazoinukia kama  ilivyoazimiwa mwaka jana kwenye mkutano wa  G8 uliofanyika  Heiligendamm -Ujerumani. Bibi Merkel amesema wakuu wa nchi na serikali wa nchi tajiri wameazimia kutekeleza jukumu la kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa.

kuhusu Afrika nchi  za G8 zimekubaliana kuendelea kuzisaidia  nchi hizo kwa kutenga kiasi cha dola Bilioni 10  za haraka. Lakini mashirika ya misaada yamesema fedha hizo hazitasaidia kitu kutokana  na mifumuko ya bei za chakula  na  nishati.

Kwenye mkutano wao  viongozi wa nchi tajir pia walijadili suala la Zimbabwe. Viongozi hao wamependekeza kumpeleka  mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini  Zimbabwe .

Nchi tajiri 8 duniani ambazo ni Marekani,Ujerumani,Ufaransa,Uingereza Japan,Canada ,Italia na Urusi zimekubaliana kutekeleza ahadi  za hapo awali juu ya kuendelea  kutoa kiasi cha dola bilioni 60 kwa ajili ya kupambana na maradhi.  Viongozi wa nchi hizo wamesema  watatekeleza ahadi walizotoa, katika kipindi cha miaka mitano ijayo.

Hapo  awali  nchi hizo  ziliahidi kutoa msaada wa dola  bilioni  25 kila  mwaka kwa ajili ya Afrika.