1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MONROVIA :Marais Hu na Sirleaf watia saini mikataba ya biashara

2 Februari 2007
https://p.dw.com/p/CCVy

Rais Hu Jintao wa China ameizuru Liberia-kituo cha pili cha ziara yake katika nchi nane barani Afrika.Kiongozi huyo wa China alikuwa na mazungumzo pamoja na rais wa Liberia Bi.Ellen Johnson Sirleaf.Viongozi hao wametia saini makubaliano ya pande mbili kuhusika na sekta za biashara,elimu na afya.Sudan,iliyo na utajiri wa mafuta,ni kituo kingine katika ziara ya rais Hu anaekabiliwa na shinikizo la kimataifa kutumia ushawishi wa China kumaliza mgogoro wa Darfur uliosababisha vifo vya zaidi ya watu 200,000 katika kipindi cha miaka minne.Inaaminiwa kuwa Beijing kama mwekezaji mkuu kabisa wa kigeni nchini Sudan,ina uwezo wa kuishawishi serikali ya Khartoum kuruhusu vikosi vya amani vya Umoja wa Mataifa kupelekwa Darfur.