1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Moscow. Vyama vinavyounga mkono serikali vyashinda uchaguzi.

12 Machi 2007
https://p.dw.com/p/CCJz

Matokeo ya mwanzo katika uchaguzi wa majimbo yameviweka vyama viwili vinavyounga mkono serikali mjini Moscow katika nafasi ya uongozi.

Chama cha United Russia, kinachoungwa mkono na rais Vladimir Putin , kinatarajiwa kuthibitishwa kushinda, wakati chama cha Fair Russia kimeonyesha uwezo mkubwa. Mashirika ya habari yanasema kuwa vyama hivyo viwili vimepata kati ya asilimia 50 na 70 ya kura.