1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mourinho: Torres bado ataichezea Chelsea

4 Aprili 2014

Kocha wa Chelsea Jose Mourinho anasisitiza kuwa Fernando Torres angali na fursa ya kuendelea kuichezea klabu hiyo licha ya kutoanza mchuano wa Champions League dhidi ya Paris St Germain.

https://p.dw.com/p/1BcGZ
Fußball Europa League Finale Chelsea Benfica Lissabon
Picha: Reuters

Mourinho alimchagua Andre Schuerrle badala ya Mhispania huyo wakati walipofungwa magoli matatu kwa moja na kisha baadaye akakiri kuwa hakufurahishwa na mchezo wa karibu wa washambuliaji wake.

Mreno huyo hajaficha lolote kuhusu nia ya Chelsea kumnunua mshambuliaji wa tajriba ya juu wakati wa kipindi kijacho cha uhamisho, na kuzusha maswali kuhusu mustakabali wa Torres.

Mourinho amesema Torres ameonyesha mchango wake tangu alipojiunga na Chelsea, lakini anaweza kuongea bidii ili kuendelea kufunga magoli. Chelsea wanacheza baadaye leo dhidi ya Stoke City wakilenga kuyafufua matumaini yao ya kutwaa taji la Premier League

Mwandishi: Bruce Amani/AFP/DPA
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman