1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MPLA yashinda uchaguzi Angola

3 Septemba 2012

Nchini Angola chama tawala cha MPLA cha rais Jose eduardo dos Santos kimetangazwa rasmi kuwa kimeshinda uchaguzi wa bunge la nchi hiyo uliofanyika Ijumaa iliyopita.

https://p.dw.com/p/162Gy
Bild: António Cascais Wann wurde das Bild gemacht?: 31.08.12 Wo wurde das Bild aufgenommen?: Luanda, Angola
Picha: DW

Vyombo vya habari vya serikali vilitangaza taarifa hiyo hata kabla ya matokeo ya mwisho kutolewa. Kwa hivyo, rais dos Santos anabakia miaka mitano zaidi madarakani.

Kutokana na mabadiliko ya katiba ya mwaka 2010 ni kwamba kiongozi wa chama kilichopata kura nyingi kabisa anakuwa rais na mkuu wa serikali.  Taarifa za Tume ya Uchaguzi iliyotangazwa katika mji mkuu wa Luanda ilitaja kwamba asilimia 75 ya wapiga kura walikichagua chama cha MPLA.

Wapiga kura wa Angola wakisubiri kushiriki uchaguzi mjini Luanda
Wapiga kura wa Angola wakisubiri kushiriki uchaguzi mjini LuandaPicha: AP

Chama kikubwa kabisa cha upinzani, UNITA, kilipata asilimia 18 ya kura. Msemaji wa upinzani na waangalizi huru wa uchaguzi hapo kabla walilalamika kwamba kulikuweko kasoro katika zoezi la uchaguzi huo. Jumla ya viti 220 vimeshindaniwa katika uchaguzi huo.

Uchaguzi umekwenda kwa amani

Mamlaka nchini humo imesema kuwa zoezi la upigaji kura limefanyika kwa amani. Huu ni uchaguzi wa tatu nchini Angola tangu ipate uhuru wake kutoka kwa Wareno mwaka 1975. Uchaguzi wa mwisho ulifanyika mwaka 2008.

Uchaguzi uliotangulia kabla ya huo wa mwaka 2008 ulifanyika mwaka 1992. Matokeo ya kutatanisha ya uchaguzi huo yalizusha awamu ya pili vya vita vya muda mrefu vya wenyewe kwa wenyewe katika taifa hilo la kusini mwa Afrika.

Kituo cha kupigia kura Angola
Kituo cha kupigia kura AngolaPicha: DW

Katika uchaguzi wa safari hii, kwa mara ya kwanza Waangola walioko nje wanaoishi nchini Ureno wamekataliwa kupiaga kura.

José Eduardo dos Santos, Rais wa Angola
José Eduardo dos Santos, Rais wa AngolaPicha: Reuters

Angola imepata mafanikio kiuchumi kutokana na mafuta. Hata hivyo wachambuzi wameonya kuwa wakati wasomi wachache wananufaika, kundi kubwa la raia wameendelea kubaki katika dimbwi la umasikini.

Mwandishi: Stumai George

Mhariri: Othman Miraji