1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mshambuliaji alilenga watumiaji mitandao ya kijamii

Sekione Kitojo
16 Machi 2019

Mshambuliaji anayetuhumiwa  kufanya  mashambulizi  nchini New Zealand  alipanga shambulizi  lake kwa  uangalifu  kwa  ajili  ya  enzi ya  mtandao  wa  internet.

https://p.dw.com/p/3FANx
Neuseeland | Anschlag von Christchurch | Gedenken
Picha: Reuters/J. Silva

 Alionesha  moja kwa  moja  mauaji  hayo, akipiga kelele  kauli  mbiu maarufu  na  kuchapisha rasimu  ndefu ikiwa  na  utani  ndani  yake  iliyolenga  wale  waliojificha  chini kwa  chini  katika  utamaduni wa  mtandao  wa  internet.

Neuseeland | Anschlag von Christchurch | Gedenken
Watu mjini Christchurch wakiweka mauaji katika eneo la maafa kama ishara ya maomboleziPicha: Reuters/E. Su

Hii  yote  inamfanya  Brenton Harrison Tarrant , mtu  aliyeshitakiwa  kwa  mauaji  kuhusiana na  shambulio  hilo la  Ijumaa  katika  misikiti  mjini  Christchurch, mtu  wa  hivi  karibuni kabisa  kudaiwa  kufanya  mauaji  makubwa  pamoja  na  wito  kwa  jamii  ya  mitandao ambayo  inazalisha  itikadi  kali.

Kabla  ya   kuuwawa  watu  sita mjini Isla Vista, Califonia, mwaka 2014, Elliott Rodger aliweka  mtandaonmi  vidio  na  kusambaza  waraka  mrefu  ukiwa  na  malalamiko  kadhaa. Baadaye aligundulika  kuwa  na  mahusiano  na  kundi  la  mtandaoni  la  misogynisti linalofahamika  kama "Incels" ama  "Involuntary celibates,"  ambao  baadhi  ya  nyakati  hutoa wito  wa  matumizi  ya  nguvu dhidi  ya  wanawake. Mwaka  jana  Robert Bowers, mtu aliyeshitakiwa  kwa  kuwauwa  watu 11  katika  sinagogi la  mjini  Pittsburgh , aliweka mtandaoni  vitisho  dhidi  ya  Gab, tovuti  ya  mtandao  wa  kijamii  unaopendelewa  na wazungu wanaoamini  kuwa  wao  ni  jamii  bora, White suprimacists.

Neuseeland | Anschlag von Christchurch | Polizei durchsucht Gegend um Moschee
Maafisa wa polisi wakijitayarisha kufanya upekuzi eneo karibu na msikiti wa Al Noor mjini Christchurch , New ZealandPicha: picture-alliance/AP Photo/M. Baker

Uandikishaji  pamoja  na  kusambaa  kwa  mawazo ya  itikadi  kali  si  kitu  kipya, kwa  mtu ama  katika  mitandao. Watu ambao  wanataka  kujadili  mawazo kama  hayo  yanauwezo wa  kujuana, amesema  Daniel Byman, mtaalamu mwandamizi  katika  taasisi  ya  Brookings. Lakini  wakati  makundi  madogo  huenda  yamekutana  mar  moja  katika  maisha  halisi, sasa  watu  wanaweza  kwenda  katika  mtandao  na  kukutana  na  makundi  makubwa kujiimarisha na  kuendeleza mawazo  yao  karibu  wakati  huo  huo.

Matendo  ya  mtandaoni

Watu  hufanya  mambo  katika  mtandao ambayo wanaweza  kusita  kufanya  katika  maisha halisi, Byman  amesema. Hii  inaweza  kuwa  kuanzia  matendo  ambayo  hayana  madhara, kama  kutuma  barua  pepe kwa  mtu  ambae huwezi  kukutana  nae katika  hafla, na kubadilishana  nae mambo, kujenga  na  kuhimiza  mawazo  ya  itikadi  kali  pamoja  na matumizi  ya  nguvu.

"Inakuwezesha kuwa  jasiri," Byman  amesema.

Wapelelezi mtandaoni haraka waliweza  kuhusisha  na  video  hiyo  iliyoonekana  moja  kwa moja  na  maandishi yaliyotolewa  na  mtumiaji  huyo  katika  8chan, kona  ya  kificho  ya tovuti  ambako  wale  ambao  hawaridhishwi  na  mitandao  ya  kijamii inayofahamika  mara nyingi  huweka  maandishi  yao  ya mawazo ya imani  kali , kibaguzi  na  matumizi  ya  nguvu.

Waraka  wa  Tarrant ulisambaa  haraka  katika  8chan  jana  Ijumaa. Waraka  huo  wenye kurasa 74 unasambaza  mawazo  ya  wazungu  wanaoamini  kuwa  wao  ni  jamii  bora hata kama  unajikanganya wenyewe. Baadhi  waliona  hali  ya  kushabihiana katika  waraka  wa kurasa  1,500 ulioandikwa  na  Anders Behring Breivik, Mnorway mwenye hisia za  siasa  kali za  mrengo  wa  kulia  ambaye  aliwauwa  watu 77  katika  mwaka  2011.

Neuseeland | Anschlag von Christchurch | Jacinda Ardern
Waziri mkuu wa New Zealand Jacinda ArdernPicha: Getty Images/M. Tantrum

Waraka 

Waraka  wa  Tarrant unaonekana  kulenga  kutoa  kwa  jamii  ya  mtandaoni  aliyoshiriki , kwa sehemu  kwa  kueleza  mada zinazofahamika  sana  katika  mtandao  wa  internet na mitazamo  wa  kejeli.

Rais Donald Trump  wa  Marekani  ameonesha  hali ya kupuuzia kuwapo  na  kitisho kinachotokana  na  uzalendo  wa  kibaguzi  wa  wazungu  baada  ya  mtu  huyo  aliyekuwa  na silaha na  kufanya  mauaji  katika  misikiti  nchini  New Zealand kumuita  rais  huyo  kuwa  "ni ishara ya utambuzi  mpya  wa  wazungu".

Trump  ambaye hatua  zake  za  kushughulikia  vuguvugu  hilo  la  wazungu zilisababisha kuangaliwa  kwa  undani, ameeleza kusikitishwa  kwake  na  wahanga  waliouwawa , katika kile  alichosema "maeneo  ya  ibada yaliyogeuzwa  maeneo  ya  mauaji ya  uovu. lakini amekataa  kujiunga  na  maelezo  ya  ongezeko  la  wasi  wasi  juu  ya  uzalendo  wa  kizungu, wakati  alipoulizwa  iwapo  anafikiri  ni  kitisho  kinachoongezeka  duniani, alijibu , "sifikiri hivyo  kwa  kweli.

Neuseeland | Anschlag von Christchurch | Brenton Tarrant
Mtuhumiwa wa mauaji Brenton Tarrant akiongozwa na polisi kuelekea mahakamaniPicha: Reuters/M. Mitchell

Wakaazi  wa  New Zealnad  walioshitushwa  na  tukio  la  mauaji  walifika  katika  maeneo wanakoishi   jamii  ya  Waislamu  katika  nchi  hiyo leo  Jumamosi, katika  dhamira  nzito kuonesha  ukarimu  wakati mtu  aliyefyatua  risasi mwenye imani  ya  kuwa  jamii  ya wazungu  ndio  jamii  bora akisimama kimya  mbele  ya  jaji , akishutumiwa  kwa  mauaji katika  misikiti  ambapo  watu 49  waliuwawa.