1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

NEW YORK:Majeshi ya Shirika kuhudumu Darfur kwa mwaka mmoja

17 Julai 2007
https://p.dw.com/p/CBhw

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon anatowa wito wa kuidhinishwa kwa haraka hatua ya kupeleka majeshi ya kulinda usalama ya Umoja wa Afrika yatakayoshirikiana na yale ya Umoja wa mataifa katika eneo la Darfur nchini Sudan.

Wiki jana Uingereza,Ufaransa na Ghana zilisambaza azimio lililodurusiwa la Baraza la usalama la umOJA WA mataia linaloidhinisha hatua hiyo.Majeshi hayo yanatarjiwa kuanza kazi kwa muda wa mwaka mmoja kwanza.