1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Neymar afungiwa kucheza mechi nne

Admin.WagnerD20 Juni 2015

Nyota wa Brazil Neymar amepigwa marufuku ya mechi nne, maana kuwa hatoweza kucheza tena katika dimba la Kombe la Mataifa ya Amerika ya Kusini, japokuwa Brazil inaweza kukata rufaa dhidi ya adhabu hiyo.

https://p.dw.com/p/1Fk4X
Chile Copa America 2015 Rote Karte von Neymar
Picha: Reuters/U. Marcelino

Shirikisho la Kandanda la Amerika Kusini Conmebol limesema uamuzi huo ulikuja baada ya mshambuliaji huyo kuonyeshwa kadi nyekundu katika mchuano wa Jumatano waliofungwa goli moja kwa bila na Colombia na “matukio yaliyofuata”. Shirikisho hilo pia limemtoza Neymar dola 10,000.

Hata ikiwa watasonga mbele katika dimba hilo hadi fainali, Brazil itakuwa na mechi nne tu zilizosalia maana kuwa Neymar atazikosa zote. Mshambuliaji wa Colombia Carlos Bacca, aliyehusika katika vurugu na Neymar amepigwa marufuku ya mechi mbili.

Mwandishi: Bruce Amani/AFP/Reuters
Mhariri: Abdu Mtullya