1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ni shida kutimiza Malengo ya Maendeleo ya Milenia

18 Juni 2010

Malengo ya Maendeleo ya Milenia ni mada mojawapo iliyojadiliwa na Bunge la Ujerumani siku ya Alkhamisi.

https://p.dw.com/p/NvKH
ARCHIV - Der damals designierte Entwicklungshilfeminister Dirk Niebel, aufgenommen am 25. Oktober 2009 waehrend des ausserordentlichen FDP-Parteitages in Berlin. Nach dem toedlichen Gefecht mit Taliban-Kaempfern nahe Kundus hat Bundesentwicklungsminister Dirk Niebel mehr Rueckhalt in der Bevoelkerung fuer den Bundeswehr-Einsatz in Afghanistan gefordert. Das Gefecht zeige, wie gefaehrlich die Situation fuer die Soldaten dort sei. "Sie wuenschen sich mehr Verstaendnis dafuer, dass sie sich, manchmal auch praeventiv, wehren muessen", sagte der FDP-Politiker nach einem Gespraech mit Bundeswehrsoldaten in Afghanistan der "Bild am Sonntag" vom 4. April 2010. (AP Photo/Eckehard Schulz, Archiv) --- FILE - Then designated German minister of economic cooperation and development Dirk Niebel is seen during the extraordinary congress of German Free Democratic Party in Berlin, Germany, in an Oct. 25, 2009 file photo. (AP Photo/Eckehard Schulz, File)
Waziri wa Misaada ya Maendeleo wa Ujerumani, Dirk Niebel.Picha: AP

Mwanzoni mwa karne hii,Umoja wa Mataifa ulijiwajibisha kupunguza kwa nusu umasikini, kote ulimwenguni ifikapo mwaka 2015. Lakini yadhihirika kuwa ni vigumu kulitekeleza lengo hilo. Hata katika sekta za afya na elimu ni hali hiyo hiyo, kwani wakati huu wa mizozo ya fedha na uchumi duniani, wafadhili wengi, ikiwemo pia Ujerumani, hawatoweza kutimiza ahadi za kusaidia kifedha.

Mwaka huu wa 2010, serikali ya Ujerumani inatenga takriban Euro bilioni sita kwa ajili ya misaada ya maendeleo. Hicho ni kiwango kikubwa lakini ni dhahiri kuwa mwaka huu, serikali ya muungano wa vyama vya kihafidhina na kiliberali haitoweza kutimiza ahadi ya serikali iliyotangulia - yaani kutoa asilimia 0.51 ya pato jumla la ndani. Msaada utakaotolewa huenda ukafikia asilimia 0.4 tu.

Hiyo haifurahishi lakini mtu anapaswa kufahamu kuwa Ujerumani haina budi kurekebisha bajeti yake iliyoathirika kutokana na msukosuko wa kiuchumi uliotokea kote duniani. Hayo alitamka Dagmar Wöhrl, mwenyekiti wa kamati ya bunge inayohusika na masuala ya maendeleo na ushirikiano wa kiuchumi. Katika mwaka huu wa 2010 pekee, Ujerumani itakuwa na deni jipya la Euro bilioni 80.Akaongezea:

" Sisi wenyewe tukiwa katika hali ya udhaifu basi hatuwezi tena kuwasaidia wengine."

Lakini, msemaji wa chama cha SPD Sascha Raabe, anayeshughulikia masuala ya misaada ya maendeleo, amelalamika kuwa waziri wa maendeleo Dirk Niebel wa chama cha kiliberali cha FDP anatenga kifungu kidogo sana cha fedha kwa ajili ya miradi ya kimataifa. Amesema:

" Yeye anataka kutoa theluthi mbili ya fedha hizo, ili Ujerumani iweze kuweka muhuri wake katika kila mradi kote duniani. Kwake, ufanisi si kuboresha hali ya walio masikini kabisa bali ni kupata kandarasi zaidi kwa biashara ya Ujerumani."

Ukweli ni kwamba waziri wa maendeleo ameanzisha mkondo mpya. Msingi ni kuwepo ushirikiano zaidi katika sekta ya uchumi - yaani katika siku zijazo,serikali ishirikiane zaidi na makampuni ya binafsi.

Kwa upande mwingine, Wöhrl anasema si wafadhili tu wanaohimizwa. Hata nchi zinazoendelea yaani zile zinazopokea misaada ya maendeleo, zinawajibishwa zaidi kuliko hapo awali, kwani sekta ya kilimo haikushughulikiwa ipasavyo na nchi hizo, tangu miongo kadhaa.

Hata hivyo,rasmi serikali ya Ujerumani inaazimia kutimiza lengo la kuongeza mchango wake wa msaada wa maendeleo hadi asilimia 0.7 ya pato jumla la ndani, ifikapo mwaka 2015.

Mwandishi:Fürstenau,Marcel/ZPR/P.Martin

Mhariri:Josephat Charo