1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Operesheni ya kijeshi Kongo yaingia siku ya pili

Thelma Mwadzaya21 Januari 2009

Nchini Kongo Rais Joseph Kabila amekutana mjini Kinshasa na mabalozi wa nchi 5 wanachama wa Baraza la kudumu la Umoja wa Mataifa kwa lengo la kuwahamasisha kuhusu operesheni za kijeshi dhidi ya waasi wa FDLR

https://p.dw.com/p/GdTu


Operesheni hizo zinaendeshwa kwa pamoja na jeshi la Kongo na lile la Rwanda.Wakati huohuo Spika wa bunge la Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo Vital Kamere ameshutumu vikali kualikwa kwa wanajeshi wa Rwanda nchini mwake.Wanajeshi hao wa Rwanda waliingia mashariki mwa Kongo mnamo siku ya Jumatatu.

Mwandishi wetu Saleh Mwanamilongo kutoka Kinshasa katuletea ripoti ifuatayo.